Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 29:15 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Fimbo na maonyo hutia hekima; Bali mwana aliyeachiliwa humwaibisha mamaye.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Adhabu na maonyo huleta hekima, lakini mtoto aliyeachwa afanye apendavyo humwaibisha mama yake.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Adhabu na maonyo huleta hekima, lakini mtoto aliyeachwa afanye apendavyo humwaibisha mama yake.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Adhabu na maonyo huleta hekima, lakini mtoto aliyeachwa afanye apendavyo humwaibisha mama yake.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Fimbo ya maonyo hutia hekima, bali mtoto asiyeonywa humwaibisha mama yake.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Fimbo ya maonyo hutia hekima, bali mtoto aliyeachiwa bila maonyo humwaibisha mama yake.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Fimbo na maonyo hutia hekima; Bali mwana aliyeachiliwa humwaibisha mamaye.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 29:15
13 Marejeleo ya Msalaba  

Tena baba yake hakumchukiza wakati wowote kwa kusema, Mbona umefanya hivi? Kisha, alikuwa mtu mzuri sana; naye alizaliwa baada ya Absalomu.


Mwana mwenye hekima humfurahisha babaye; Bali mwana mpumbavu ni mzigo wa mamaye.


Akusanyaye wakati wa joto ni mwana mwenye hekima; Bali asinziaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.


Yeye asiyetumia fimbo yake humchukia mwanawe; Bali yeye ampendaye humrudi mapema.


Azaaye mpumbavu ni kwa huzuni yake mwenyewe; Wala baba wa mpumbavu hana furaha.


Mwana mpumbavu ni huzuni kwa babaye, Na uchungu kwa mamaye aliyemzaa.


Mrudi mwanao, kwa maana liko tumaini; Wala usiikaze nafsi yako kwa kuangamia kwake.


Ujinga umefungwa ndani ya moyo wa mtoto; Lakini fimbo ya adhabu itaufukuzia mbali.


Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee.


Mrudi mwanao naye atakustarehesha; Naam, atakufurahisha nafsi yako.


Amwendekezaye mtumwa wake tangu utoto, Mwisho wake atakuwa ni mwanawe.