Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 23:23 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Inunue kweli, wala usiiuze; Naam, hekima, na mafundisho, na ufahamu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Nunua ukweli, wala usiuuze; nunua hekima, mafunzo na busara.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Nunua ukweli, wala usiuuze; nunua hekima, mafunzo na busara.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Nunua ukweli, wala usiuuze; nunua hekima, mafunzo na busara.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Nunua kweli wala usiiuze, pata hekima, adabu na ufahamu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Nunua kweli wala usiiuze, pata hekima, adabu na ufahamu.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Inunue kweli, wala usiiuze; Naam, hekima, na mafundisho, na ufahamu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 23:23
19 Marejeleo ya Msalaba  

Ndiyo maana nimeyapenda maagizo yako, Kuliko dhahabu, naam, dhahabu iliyo safi.


Sheria ya kinywa chako ni njema kwangu, Kuliko maelfu ya dhahabu na fedha.


Mwana mwenye hekima humfurahisha babaye; Bali mwana mpumbavu ni mzigo wa mamaye.


Si afadhali kupata hekima kuliko dhahabu? Naam, yafaa kuchagua ufahamu kuliko fedha.


Nini maana yake, mpumbavu kuwa na fedha mkononi mwake ya kununulia hekima, Ikiwa hana moyo wa ufahamu?


Moyo wa mwenye busara hupata maarifa; Na sikio la mwenye hekima hutafuta maarifa.


Usimkaripie mwenye dharau, asije akakuchukia; Mkaripie mwenye hekima, naye atakupenda.


Haya, kila aonaye kiu, njoni majini, Naye asiye na fedha; njoni, nunueni mle; Naam, njoni, nunueni divai na maziwa, Bila fedha na bila gharama.


Tena ufalme wa mbinguni umefanana na hazina iliyositirika katika shamba; ambayo mtu alipoiona, aliificha; na kwa furaha yake akaenda akauza alivyo navyo vyote, akalinunua shamba lile.


naye alipoona lulu moja ya thamani kubwa, alikwenda akauza alivyo navyo vyote, akainunua.


Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kuipoteza nafsi yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?


isipokuwa Roho Mtakatifu mji kwa mji hunishuhudia akisema, ya kwamba vifungo na dhiki vyaningoja.


akihesabu ya kuwa kushutumiwa kwake Kristo ni utajiri mkuu kuliko hazina za Misri; kwa kuwa aliyatazamia hayo malipo.


Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa.


Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona.