Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 22:9 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Mwenye jicho la ukarimu atabarikiwa; Maana huwapa maskini chakula chake.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mtu mkarimu atabarikiwa, maana chakula chake humgawia maskini.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mtu mkarimu atabarikiwa, maana chakula chake humgawia maskini.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mtu mkarimu atabarikiwa, maana chakula chake humgawia maskini.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Mtu mkarimu yeye mwenyewe atabarikiwa kwa kuwa hushiriki chakula chake na maskini.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Mtu mkarimu yeye mwenyewe atabarikiwa kwa kuwa hushiriki chakula chake na maskini.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Mwenye jicho la ukarimu atabarikiwa; Maana huwapa maskini chakula chake.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 22:9
29 Marejeleo ya Msalaba  

Ametoa kwa ukarimu, na kuwapa maskini, Haki yake yakaa milele, Pembe yake itatukuzwa kwa utukufu.


Mwenye rehema huitendea mema nafsi yake; Aliye mkali hujisumbua mwili wake.


Nafsi ya mtu mkarimu itastawishwa; Anyweshaye atanyweshwa mwenyewe.


Atafutaye mema kwa bidii hutafuta fadhili; Atafutaye madhara, hayo yatamjia.


Amdharauye mwenzake afanya dhambi; Bali amhurumiaye maskini ana heri.


Amhurumiaye maskini humkopesha BWANA; Naye atamlipa kwa tendo lake jema.


Azibaye masikio yake asisikie kilio cha maskini, Yeye naye atalia, lakini hatasikiwa.


Aibaye mali ya babaye au mamaye, na kusema, Si kosa; Mwana huyo ni rafiki wa mtu mharibifu.


Mwenye kuwagawia maskini hatahitaji kitu; Bali afichaye macho yake atakuwa na laana nyingi.


Huwakunjulia maskini mikono yake; Naam, huwanyoshea wahitaji mikono yake.


Bali muungwana huwaza mambo ya kiungwana, naye hushika sana mambo ya kiungwana.


Si halali yangu kutumia vilivyo vyangu kama nipendavyo? Au jicho lako limekuwa ovu kwa sababu ya mimi kuwa mwema?


wizi, uuaji, uzinzi, tamaa mbaya, ukorofi, hila, ufisadi, kijicho, matukano, kiburi, upumbavu.


Bali ufanyapo karamu waite maskini, vilema, viwete, vipofu,


Katika mambo yote nimewaonesha ya kuwa kwa kushika kazi hivi imewapasa kuwasaidia wanyonge, na kuyakumbuka maneno ya Bwana Yesu, jinsi alivyosema mwenyewe, Ni heri kutoa kuliko kupokea.


Mwanamke kati yenu aliye mwororo na laini, ambaye hangehatarisha kuweka wayo wa mguu wake nchi kwa umalidadi na ulaini, jicho lake huyu litakuwa ovu juu ya mume wa kifuani mwake, na juu ya mwanawe, na juu ya binti yake,


Lakini msisahau kutenda mema na kushirikiana; maana sadaka kama hizi ndizo zimpendezazo Mungu.


Maana Mungu si dhalimu hata aisahau kazi yenu, na pendo lile mlilolidhihirisha kwa jina lake, kwa kuwa mmewahudumia watakatifu, na hata hivi sasa mngali mkiwahudumia.


Mkaribishane ninyi kwa ninyi, pasipo kunung'unika;