Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 20:13 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Usipende usingizi usije ukawa maskini; Fumbua macho yako nawe utashiba chakula.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Usipende kulala tu usije ukawa maskini; uwe macho nawe utakuwa na chakula kingi.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Usipende kulala tu usije ukawa maskini; uwe macho nawe utakuwa na chakula kingi.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Usipende kulala tu usije ukawa maskini; uwe macho nawe utakuwa na chakula kingi.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Usiupende usingizi la sivyo utakuwa maskini, uwe macho nawe utakuwa na chakula cha akiba.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Usiupende usingizi la sivyo utakuwa maskini, uwe macho nawe utakuwa na chakula cha akiba.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Usipende usingizi usije ukawa maskini; Fumbua macho yako nawe utashiba chakula.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 20:13
15 Marejeleo ya Msalaba  

Atendaye mambo kwa mkono mlegevu huwa maskini; Bali mkono wake aliye na bidii hutajirisha.


Alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele; Bali afuataye mambo ya upuzi hana ufahamu.


Nafsi ya mtu mvivu hutamani asipate kitu; Bali nafsi ya mwenye bidii itanenepeshwa.


Uvivu humtia mtu katika usingizi mzito; Na nafsi yake mvivu itaona njaa.


Haifai kitu, haifai kitu, asema mnunuzi; Lakini akiisha kwenda zake hujisifu.


Alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele; Bali afuataye mambo ya upuzi atapata umaskini wa kumtosha.


Tena huamka, kabla usiku haujaisha; Huwapa watu wa nyumbani mwake chakula; Na wajakazi wake sehemu zao.


Basi nahodha akamwendea, akamwambia, Una nini, Ewe ulalaye usingizi? Amka, ukamwombe Mungu wako; labda Mungu huyo atatukumbuka, tusipotee.


kwa bidii, bila kulegea; mkiwa na juhudi katika roho zenu; mkimtumikia Bwana;


Naam, tukiujua wakati, kwamba saa ya kuamka katika usingizi imekwisha kuwadia; kwa maana sasa wokovu wetu uko karibu nasi kuliko tulipoanza kuamini


Tumieni akili kama ipasavyo, wala msitende dhambi; kwa maana wengine hawamjui Mungu. Ninanena hayo niwafedheheshe.


Hivyo husema, Amka, wewe usinziaye, Ufufuke katika wafu, Na Kristo atakuangaza.


Kwa kuwa hata wakati ule tulipokuwapo kwenu tuliwaagiza neno hili, kwamba ikiwa mtu hataki kufanya kazi, basi, asile chakula.