Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 17:13 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Yeye arudishaye mabaya badala ya mema, Mabaya hayataondoka nyumbani mwake.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mwenye kulipiza mema kwa mabaya, mabaya hayataondoka nyumbani mwake.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mwenye kulipiza mema kwa mabaya, mabaya hayataondoka nyumbani mwake.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mwenye kulipiza mema kwa mabaya, mabaya hayataondoka nyumbani mwake.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Ikiwa mtu atalipa baya kwa jema, kamwe ubaya hautaondoka katika nyumba yake.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Ikiwa mtu atalipa baya kwa jema, kamwe ubaya hautaondoka katika nyumba yake.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Yeye arudishaye mabaya badala ya mema, Mabaya hayataondoka nyumbani mwake.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 17:13
18 Marejeleo ya Msalaba  

Basi, sasa upanga hautaondoka nyumbani mwako, kwa sababu umenidharau, ukamtwaa mkewe Uria, Mhiti, kuwa mke wako.


Kisha nitaifanya nyumba yako iwe kama nyumba ya Yeroboamu mwana wa Nebati, na kama nyumba ya Baasha mwana wa Ahiya, kwa ajili ya chukizo ulilonichukiza, hata kunighadhibisha, ukawakosesha Israeli.


Wananilipa mabaya badala ya mema, Hata nafsi yangu ikaingia ukiwa.


Naam, wakilipa mabaya kwa mema, Huwa adui zangu kwa kuwa nilifuata lililo jema.


Uovu huwafuatia wenye dhambi; Bali mwenye haki atalipwa mema.


Watu wote wakajibu wakasema, Damu yake na iwe juu yetu, na juu ya watoto wetu.


Akavitupa vile vipande vya fedha katika hekalu, akaondoka; akaenda, akajinyonga.


Msimlipe mtu ovu kwa ovu. Angalieni yaliyo mema machoni pa watu wote.


Angalieni mtu awaye yote asimlipe mwenziwe mabaya kwa mabaya; bali siku zote lifuateni lililo jema, ninyi kwa ninyi na kwa watu wote.


watu wasiolipa baya kwa baya, au laumu kwa laumu; bali wenye kubariki; kwa sababu hayo ndiyo mliyoitiwa ili mrithi baraka.


Naye Yonathani akamsifu Daudi kwa Sauli, babaye akamwambia, Mfalme asikose juu ya mtumishi wake, yaani, juu ya Daudi kwa maana yeye hakukosa juu yako, tena matendo yake kwako yamekuwa mema sana.


Akamwambia Daudi, Wewe u mwenye haki kuliko mimi; maana wewe umenitendea mema, nami nimekutenda mabaya.


Basi Daudi alikuwa amesema, Hakika ni bure nilivyokuwa nikilinda nyikani yote aliyo nayo mtu huyu, asipotewe na kitu chochote cha mali yake yote; naye amenilipa mabaya badala ya mema.