Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 16:31 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Kichwa chenye mvi ni taji la utukufu, Kama kikionekana katika njia ya haki.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Kuwa na mvi za uzee ni taji la utukufu; hupatikana kwa maisha ya uadilifu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Kuwa na mvi za uzee ni taji la utukufu; hupatikana kwa maisha ya uadilifu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Kuwa na mvi za uzee ni taji la utukufu; hupatikana kwa maisha ya uadilifu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Mvi ni taji la utukufu; hupatikana kwa maisha ya uadilifu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Mvi ni taji ya utukufu; hupatikana kwa maisha ya uadilifu.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Kichwa chenye mvi ni taji la utukufu, Kama kikionekana katika njia ya haki.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 16:31
16 Marejeleo ya Msalaba  

Hufanya mapito yake kung'aa nyuma yake Hata mtu angedhani kilindi kina mvi.


Afumbaye macho, kusudi lake ni kuwaza yaliyopotoka; Aikazaye midomo yake hutokeza mabaya.


Asiye mwepesi wa hasira ni mwema kuliko shujaa; Na mtu aitawalaye roho yake kuliko mtu atekaye mji.


Wana wa wana ndio taji la wazee, Na utukufu wa watoto ni baba zao.


Fahari ya vijana ni nguvu zao, Na uzuri wa wazee ni kichwa chenye mvi.


Naam, wataogopa kilichoinuka Na vitisho vitakuwapo njiani; Na mlozi utachanua maua; Na panzi atakuwa ni mzigo mzito; Na pilipili hoho itapasuka; Maana mtu aiendea nyumba yake ya milele, Nao waombolezao wazunguka njiani.


Heri kijana maskini mwenye hekima Kuliko mfalme mzee mpumbavu ambaye hajui tena kupokea maonyo.


Mwondokeeni mtu mwenye mvi; heshimuni uso wa mtu mzee; nawe mche Mungu wako, Mimi ndimi BWANA.


Na wote wawili walikuwa wenye haki mbele za Mungu, wakiishi katika amri zote za Bwana na maagizo yake bila lawama.


lakini, kwa ajili ya upendo nakusihi, kwa kuwa ndimi, Paulo mzee, na sasa mfungwa wa Kristo Yesu pia.