Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 15:18 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Mtu wa hasira huchochea ugomvi; Bali asiye mwepesi wa hasira hutuliza mashindano.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mtu wa hasira mbaya husababisha ugomvi, lakini asiye mwepesi wa hasira hutuliza ugomvi.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mtu wa hasira mbaya husababisha ugomvi, lakini asiye mwepesi wa hasira hutuliza ugomvi.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mtu wa hasira mbaya husababisha ugomvi, lakini asiye mwepesi wa hasira hutuliza ugomvi.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Mtu mwepesi wa hasira huchochea ugomvi, bali mtu mvumilivu hutuliza ugomvi.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Mtu mwepesi wa hasira huchochea ugomvi, bali mtu mvumilivu hutuliza ugomvi.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Mtu wa hasira huchochea ugomvi; Bali asiye mwepesi wa hasira hutuliza mashindano.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 15:18
21 Marejeleo ya Msalaba  

Hao watu wa Israeli wakawajibu watu wa Yuda, wakasema, Sisi tunazo sehemu kumi katika mfalme, tena tunayo haki yetu katika Daudi zaidi kuliko ninyi; mbona basi ninyi mmetudharau sisi, msitake ushauri wetu kwanza katika kumrudisha tena mfalme wetu? Na maneno ya watu wa Yuda yakawa makali kuliko maneno ya watu wa Israeli.


Kuchukiana huleta fitina; Bali kupendana husitiri makosa yote.


Asiye mwepesi wa hasira ana fahamu nyingi; Bali mwenye roho ya hamaki hutukuza upumbavu.


Jawabu la upole hugeuza hasira; Bali neno liumizalo huchochea ghadhabu.


Njia ya mtu mvivu ni kama boma la miiba; Bali mapito yao wenye unyofu hufanyika njia kuu.


Hasira ya mfalme ni kama wajumbe wa mauti; Lakini mtu mwenye hekima ataituliza.


Mtu mshupavu huleta fitina; Na mchongezi huwafarakanisha rafiki.


Usifanye urafiki na mtu mwenye hasira nyingi; Wala usiende na mtu wa ghadhabu nyingi;


Kwa uvumilivu mwingi mkuu husadikishwa; Na ulimi laini huvunja mfupa.


Kama makaa juu ya makaa yanayowaka, Na kama kuni juu ya moto; Ndivyo mtu mgomvi achocheavyo uadui.


Mwenye nafsi ya kutamani huchochea fitina; Bali amtumainiye BWANA ataneemeshwa.


Mtu wa hasira huchochea ugomvi; Na mtu mwenye ghadhabu huasi sana.


Roho yake mtawala ikiinuka kinyume chako, Usiondoke mara mahali pako ulipo; Kwa maana roho ya upole hutuliza machukizo yaliyo makubwa.


Heri wapatanishi; Maana hao wataitwa wana wa Mungu.