Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 14:35 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Upendeleo wa mfalme humwelekea mtumwa atendaye kwa busara; Bali hasira yake itakuwa juu yake aletaye aibu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mfalme humfadhili mtumishi atendaye kwa hekima, lakini hasira yake huwakumba watendao yasiyofaa.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mfalme humfadhili mtumishi atendaye kwa hekima, lakini hasira yake huwakumba watendao yasiyofaa.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mfalme humfadhili mtumishi atendaye kwa hekima, lakini hasira yake huwakumba watendao yasiyofaa.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Mfalme hupendezwa na mtumishi mwenye hekima, bali ghadhabu yake humwangukia mtumishi mwenye kuaibisha.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Mfalme hupendezwa na mtumishi mwenye hekima, bali ghadhabu yake humwangukia mtumishi mwenye kuaibisha.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Upendeleo wa mfalme humwelekea mtumwa atendaye kwa busara; Bali hasira yake itakuwa juu yake aletaye aibu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 14:35
18 Marejeleo ya Msalaba  

Farao akawaambia watumishi wake, Tupate wapi mtu kama huyu, mwenye Roho ya Mungu ndani yake?


Mfalme akaondoka kwa ghadhabu kutoka kwenye karamu ya divai, akaingia bustani ya ngome. Hamani naye akasimama ili ajitakie maisha yake kwa malkia Esta; kwa kuwa aliona ya kwamba amekusudiwa madhara na mfalme.


Akusanyaye wakati wa joto ni mwana mwenye hekima; Bali asinziaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.


Haki huinua taifa; Bali dhambi ni aibu ya watu wowote.


Midomo ya haki ni furaha ya wafalme; Nao humpenda yeye asemaye yaliyo sawa.


Mtumwa atendaye kwa busara atamtawala mwana atendaye mambo ya aibu; Tena atapata sehemu ya urithi kati ya ndugu.


Apotezaye mali za babaye na kumfukuza mamaye, Ni mwana aaibishaye, na kuleta lawama.


Mfalme mwenye hekima huwapepeta wasio haki; Naye hulipitisha gurudumu la kupuria juu yao.


Mfalme aketiye katika kiti cha hukumu, Huyapepeta mabaya yote kwa macho yake.


Apendaye usafi wa moyo, na neema ya midomo; Mfalme atakuwa rafiki yake.


Mwondoe asiye haki mbele ya mfalme, Na kiti chake cha enzi kitathibitika katika haki.


Mwenye kutawala akisikiliza uongo; Basi watumishi wake wote watakuwa waovu.


Bwana wake akamwambia, Vema, mtumwa mwema na mwaminifu; ulikuwa mwaminifu kwa machache, nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana wako.


Bwana wake akamwambia, Vema, mtumwa mwema na mwaminifu; ulikuwa mwaminifu kwa machache, nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana wako.