Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 14:31 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Amwoneaye maskini humsuta Muumba wake; Bali yeye awahurumiaye wahitaji humheshimu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Anayemdhulumu maskini anamtukana Muumba wake, lakini amwoneaye huruma mhitaji anamtukuza Mungu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Anayemdhulumu maskini anamtukana Muumba wake, lakini amwoneaye huruma mhitaji anamtukuza Mungu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Anayemdhulumu maskini anamtukana Muumba wake, lakini amwoneaye huruma mhitaji anamtukuza Mungu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Yeye anayemdhulumu maskini humdharau Muumba wao, bali yeyote anayemhurumia mhitaji humheshimu Mungu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Yeye amwoneaye maskini huonyesha dharau kwa Muumba wao, bali yeyote anayemhurumia mhitaji humheshimu Mungu.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Amwoneaye maskini humsuta Muumba wake; Bali yeye awahurumiaye wahitaji humheshimu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 14:31
19 Marejeleo ya Msalaba  

Humgeuza mhitaji aiache njia; Maskini wa nchi hujificha pamoja.


Kwa ajili ya kuonewa kwao wanyonge, Kwa ajili ya kuugua kwao wahitaji, Sasa nitasimama, asema BWANA, Nitamweka salama yeye wanayemfyonya.


Amdharauye mwenzake afanya dhambi; Bali amhurumiaye maskini ana heri.


Amchekaye maskini humtukana Muumba wake; Naye aufurahiaye msiba hatakosa adhabu.


Amhurumiaye maskini humkopesha BWANA; Naye atamlipa kwa tendo lake jema.


Yeye awaoneaye maskini ili kuongeza mapato, Naye ampaye tajiri, hupata hasara.


Tajiri na maskini hukutana pamoja; BWANA ndiye aliyewaumba wote wawili.


Yeye azidishaye mali yake kwa riba na faida, Humkusanyia mtu awahurumiaye maskini.


Ujapokuwa unaona maskini kuonewa, na hukumu na haki kuondolewa kwa jeuri katika jimbo, usilistaajabie jambo hilo; kwa sababu, Aliye Juu kuliko walio juu huangalia; Tena wako walio juu kupita hao.


Wala msidanganyane; lakini utamcha Mungu wako; kwa kuwa mimi ndimi BWANA, Mungu wenu.


Na ikiwa ndugu yako amekuwa maskini, na mkono wake umelegea kwako, ndipo utamsaidia, atakaa nawe kama mgeni, na msafiri.


Kwa maana maskini mnao sikuzote pamoja nanyi; bali mimi hamko nami sikuzote.


Usimwonee mtumishi mwenye ujira aliye maskini na uhitaji, kama ni wa nduguzo, au kama ni wageni wako mmojawapo walio katika nchi yako, ndani ya malango yako;


Na amri hii tumepewa na yeye, ya kwamba yeye ampendaye Mungu, ampende na ndugu yake.