Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 14:21 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Amdharauye mwenzake afanya dhambi; Bali amhurumiaye maskini ana heri.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Anayemdharau jirani yake ni mwenye dhambi, bali ana heri aliye mwema kwa maskini.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Anayemdharau jirani yake ni mwenye dhambi, bali ana heri aliye mwema kwa maskini.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Anayemdharau jirani yake ni mwenye dhambi, bali ana heri aliye mwema kwa maskini.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Yeye anayemdharau jirani yake hutenda dhambi, bali amebarikiwa yeye aliye na huruma kwa mhitaji.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Yeye anayemdharau jirani yake hutenda dhambi, bali amebarikiwa yeye aliye na huruma kwa mhitaji.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Amdharauye mwenzake afanya dhambi; Bali amhurumiaye maskini ana heri.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 14:21
28 Marejeleo ya Msalaba  

Heri atendaye fadhili na kukopesha; Atengenezaye mambo yake kwa haki.


Ametoa kwa ukarimu, na kuwapa maskini, Haki yake yakaa milele, Pembe yake itatukuzwa kwa utukufu.


Maana hapuuzi Wala kuchukizwa na mateso ya anayeteswa, Wala hamfichi uso wake, Bali humsikia akimlilia.


Asiye na akili humdharau mwenziwe; Bali mtu aliye na ufahamu hunyamaza.


Amwoneaye maskini humsuta Muumba wake; Bali yeye awahurumiaye wahitaji humheshimu.


Amchekaye maskini humtukana Muumba wake; Naye aufurahiaye msiba hatakosa adhabu.


Ajapo asiye haki, huja dharau pia; Na pamoja na aibu huja lawama.


Amhurumiaye maskini humkopesha BWANA; Naye atamlipa kwa tendo lake jema.


Nafsi ya mtu mbaya hutamani uovu; Jirani yake hapati fadhili machoni pake.


Mwenye jicho la ukarimu atabarikiwa; Maana huwapa maskini chakula chake.


Mwenye kuwagawia maskini hatahitaji kitu; Bali afichaye macho yake atakuwa na laana nyingi.


Yeye azidishaye mali yake kwa riba na faida, Humkusanyia mtu awahurumiaye maskini.


Kwa sababu hiyo, Ee mfalme, shauri langu lipate kibali kwako; uache dhambi zako kwa kutenda haki, uache maovu yako kwa kuwahurumia maskini; huenda ukapata kuzidishiwa siku zako za fanaka.


Akawaambia mfano huu watu waliojiamini ya kuwa wao ni wenye haki, wakiwadharau wengine wote.


Katika mambo yote nimewaonesha ya kuwa kwa kushika kazi hivi imewapasa kuwasaidia wanyonge, na kuyakumbuka maneno ya Bwana Yesu, jinsi alivyosema mwenyewe, Ni heri kutoa kuliko kupokea.


Jitunze, msiwe na neno lisilofaa moyoni mwako, kusema, Umekaribia mwaka wa saba, mwaka wa maachilio; jicho lako likawa ovu juu ya nduguyo usimpe kitu; naye akamlilia BWANA juu yako, ikawa ni dhambi kwako.


ili msiwe wavivu, bali mkawe kama hao wazirithio ahadi kwa imani na uvumilivu.