Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 11:12 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Asiye na akili humdharau mwenziwe; Bali mtu aliye na ufahamu hunyamaza.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Anayemdharau jirani yake hana akili, mtu mwenye busara hukaa kimya.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Anayemdharau jirani yake hana akili, mtu mwenye busara hukaa kimya.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Anayemdharau jirani yake hana akili, mtu mwenye busara hukaa kimya.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Mtu asiye na akili humdharau jirani yake, bali mtu mwenye ufahamu huuzuia ulimi wake.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Mtu asiye na akili humdharau jirani yake, bali mtu mwenye ufahamu huuzuia ulimi wake.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Asiye na akili humdharau mwenziwe; Bali mtu aliye na ufahamu hunyamaza.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 11:12
15 Marejeleo ya Msalaba  

Lakini hao watu wakanyamaza kimya; wala hawakumjibu hata neno moja; maana amri ya mfalme ilikuwa kwamba, Msimjibu neno.


Katika wingi wa maneno hapakosi kuwa na maovu; Bali yeye azuiaye midomo yake hufanya akili.


Mji hutukuzwa kwa mbaraka wa mwenye haki; Bali mji hupinduliwa kwa kinywa cha mwovu.


Mwenye udaku hupitapita akifunua siri; Bali mwenye roho ya uaminifu husitiri mambo.


Amdharauye mwenzake afanya dhambi; Bali amhurumiaye maskini ana heri.


Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake.


Basi Mafarisayo, ambao wenyewe ni wapenda fedha, waliyasikia hayo yote, wakamdhihaki.


Akawaambia mfano huu watu waliojiamini ya kuwa wao ni wenye haki, wakiwadharau wengine wote.


Yeye alipotukanwa, hakurudisha matukano; alipoteswa, hakutisha; bali alijikabidhi kwake yeye ahukumuye kwa haki.


Ndipo Zebuli akamwambia, Je! Kinywa chako sasa kiko wapi, hata ukasema, Huyo Abimeleki ni nani, hata inatupasa kumtumikia yeye? Je! Hawa sio majeshi hao uliowadharau wewe? Haya, toka nje sasa, tafadhali, upigane nao.


Lakini wengine wasiofaa kitu wakasema, Huyu je! Atatuokoaje? Nao wakamdharau, wasimletee zawadi.