Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Methali 1:18 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Na hao hujiotea damu yao wenyewe, Hujinyemelea nafsi zao wenyewe.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Wao huvizia na kujiangamiza wao wenyewe, hutega mtego wa kujinasa wao wenyewe.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Wao huvizia na kujiangamiza wao wenyewe, hutega mtego wa kujinasa wao wenyewe.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Wao huvizia na kujiangamiza wao wenyewe, hutega mtego wa kujinasa wao wenyewe.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Watu hawa huvizia kumwaga damu yao wenyewe; hujivizia tu wenyewe!

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Watu hawa huvizia kumwaga damu yao wenyewe; hujivizia tu wenyewe!

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Na hao hujiotea damu yao wenyewe, Hujinyemelea nafsi zao wenyewe.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Methali 1:18
13 Marejeleo ya Msalaba  

Basi wakamtundika Hamani juu ya mti aliomwekea tayari Mordekai. Ghadhabu ya mfalme ikatulia.


Nawe, Ee Mungu, utawateremsha, Wafikie shimo la uharibifu; Watu wa damu na hila hawataishi nusu ya siku zao, Bali mimi nitakutumaini Wewe.


BWANA amejidhihirisha na kutekeleza hukumu; Amemnasa mdhalimu kwa kazi ya mikono yake.


Wakisema, Haya! Njoo pamoja nasi, Na tuvizie ili kumwaga damu; Tumwotee asiye na hatia, bila sababu;


Kwa kuwa mtego hutegwa bure, Mbele ya macho ya ndege yeyote.


Haki huelekea uzima; Afuataye maovu hufuata mauti yake mwenyewe.


Haki yake mtu mkamilifu itamwongoza njia yake; Bali mtu mwovu ataanguka kwa uovu wake.


Aliyelemewa na damu ya mtu Atalikimbilia shimo; wala mtu asimzuie.


Bali kwa kadiri ya ugumu wako, na kwa moyo wako usio na toba, wajiwekea akiba ya hasira kwa siku ile ya hasira na ufunuo wa hukumu ya haki ya Mungu,