Sisi sote kama kondoo tumepotea; Kila mmoja wetu amegeukia njia yake mwenyewe; Na BWANA ameweka juu yake Maovu yetu sisi sote.
Mathayo 15:24 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC Akajibu, akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli. Matoleo zaidiBiblia Habari Njema Yesu akajibu, “Sikutumwa ila kwa watu wa Israeli waliopotea kama kondoo.” Biblia Habari Njema - BHND Yesu akajibu, “Sikutumwa ila kwa watu wa Israeli waliopotea kama kondoo.” Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza Yesu akajibu, “Sikutumwa ila kwa watu wa Israeli waliopotea kama kondoo.” Neno: Bibilia Takatifu Isa akajibu, “Nimetumwa tu kwa ajili ya kondoo wa Israeli waliopotea.” Neno: Maandiko Matakatifu Isa akajibu, “Nimetumwa tu kwa ajili ya kondoo wa Israeli waliopotea.” BIBLIA KISWAHILI Akajibu, akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli. |
Sisi sote kama kondoo tumepotea; Kila mmoja wetu amegeukia njia yake mwenyewe; Na BWANA ameweka juu yake Maovu yetu sisi sote.
Nami nitawatafuta waliopotea, nitawarudisha waliotangatanga, nitawatibu waliojeruhiwa, nitawatia nguvu wagonjwa; nao wanono na wenye nguvu nitawaharibu; nitawalisha hukumu.
Nami nitaweka mchungaji mmoja juu yao, naye atawalisha, naam, mtumishi wangu, Daudi; yeye atawalisha, naye atakuwa mchungaji wao.
Wala yeye hakumjibu neno. Nao wanafunzi wake wakamwendea, wakamwomba, wakisema, Mwache aende zake; kwa kuwa anaendelea kutupigia makelele nyuma yetu.
Na alipowaona makutano, aliwahurumia, kwa sababu walikuwa wamechoka na kutawanyika kama kondoo wasio na mchungaji.
Paulo na Barnaba wakanena kwa ushujaa wakasema, Ilikuwa lazima neno la Mungu linenwe kwenu kwanza; lakini kwa kuwa mnalisukumia mbali, na kujiona ninyi wenyewe kuwa hamkustahili uzima wa milele, angalieni, twawageukia Mataifa.
Kwa maana nasema, ya kwamba Kristo amefanyika mhudumu wa agano la kutahiriwa kwa ajili ya kweli ya Mungu, kusudi azithibitishe ahadi walizopewa baba zetu;