Matendo 14:16 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC ambaye zamani zilizopita aliwaacha mataifa yote waende katika njia zao wenyewe. Matoleo zaidiBiblia Habari Njema Zamani Mungu aliruhusu kila taifa lifanye lilivyopenda. Biblia Habari Njema - BHND Zamani Mungu aliruhusu kila taifa lifanye lilivyopenda. Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza Zamani Mungu aliruhusu kila taifa lifanye lilivyopenda. Neno: Bibilia Takatifu Zamani aliwaachia mataifa waishi walivyotaka. Neno: Maandiko Matakatifu Zamani aliwaachia mataifa waishi walivyotaka. BIBLIA KISWAHILI ambaye zamani zilizopita aliwaacha mataifa yote waende katika njia zao wenyewe. |
Kwa maana mataifa yote watakwenda, kila moja kwa jina la mungu wake, na sisi tutakwenda kwa jina la BWANA, Mungu wetu, milele na milele.
Basi, zamani zile za ujinga Mungu alijifanya kama hazioni; bali sasa anawaagiza watu wote wa kila mahali watubu.
Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa.
ambaye Mungu amekwisha kumweka awe upatanisho kwa njia ya imani katika damu yake, ili aoneshe haki yake, kwa sababu ya kuziachilia katika ustahimili wa Mungu dhambi zote zilizotangulia kufanywa;
kwamba zamani zile mlikuwa hamna Kristo, mmefarakana na jamii ya Israeli, wageni wasio wa maagano ya ahadi ile. Mlikuwa hamna tumaini, hamna Mungu duniani.
Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuishi katika uzinzi, tamaa, ulevi, na karamu za kula na kunywa vileo kupindukia, na ibada haramu ya sanamu;