Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Luka 6:29 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Akupigaye shavu moja, mgeuzie la pili, naye akunyang'anyaye joho yako, usimzuilie na kanzu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mtu akikupiga shavu moja mgeuzie pia la pili. Mtu akikunyanganya koti lako mwachie pia shati lako.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mtu akikupiga shavu moja mgeuzie pia la pili. Mtu akikunyanganya koti lako mwachie pia shati lako.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mtu akikupiga shavu moja mgeuzie pia la pili. Mtu akikunyang'anya koti lako mwachie pia shati lako.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Kama mtu akikupiga shavu moja, mgeuzie na la pili pia. Mtu akikunyang’anya koti lako, usimzuie kuchukua joho pia.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Kama mtu akikupiga shavu moja, mgeuzie na la pili pia. Mtu akikunyang’anya koti lako, usimzuie kuchukua joho pia.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Akupigaye shavu moja, mgeuzie la pili, naye akunyang'anyaye joho yako, usimzuilie na kanzu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Luka 6:29
15 Marejeleo ya Msalaba  

Naye Mefiboshethi akamwambia mfalme, Naam, hata yote na atwae yeye, kwa kuwa bwana wangu mfalme amekuja kwa amani nyumbani kwake.


Ndipo akakaribia Sedekia mwana wa Kenaana, akampiga Mikaya kofi la shavu, akasema, Alitokaje kwangu Roho ya BWANA ili aseme na wewe?


Niliwatolea wapigao mgongo wangu, na wang'oao ndevu mashavu yangu; sikuficha uso wangu usipate fedheha na kutemewa mate.


Na amwelekezee yule ampigaye shavu lake; Ashibishwe mashutumu.


Sasa utajikusanya vikosi vikosi, Ee binti wa vikosi; yeye amemhusuru; watampiga mwamuzi wa Israeli shavuni mwake kwa fimbo.


Ndipo wakamtemea mate usoni, wakampiga ngumi; na wengine wakampiga makofi,


Wakamfunika macho, kisha wakamwulizauliza wakisema, Tabiri, ni nani aliyekupiga?


Mpe kila akuombaye, na akunyang'anyaye vitu vyako, usitake akurudishie.


Basi aliposema hayo, mtumishi mmojawapo aliyesimama karibu alimpiga Yesu kofi akisema, Wamjibu hivi Kuhani Mkuu?


Kuhani Mkuu Anania akawaamuru wale waliosimama karibu naye wampige kinywa chake.


Hata saa hii ya sasa, tuna njaa na kiu, tuko uchi, twapigwa ngumi, tena hatuna makao;


Basi imekuwa upungufu kwenu kabisa kwamba mnashitakiana ninyi kwa ninyi. Maana si afadhali kudhulumiwa? Maana si afadhali kunyang'anywa mali zenu?


Maana mwachukuliana na mtu akiwatia utumwani, akiwameza, akiwateka nyara, akijikuza, akiwapiga usoni.


Maana mliwaonea huruma wale waliokuwa katika vifungo, tena mkakubali kwa furaha kunyang'anywa mali zenu, mkijua kwamba nafsini mwenu mna mali iliyo njema zaidi, idumuyo.