Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Kutoka 26:30 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Nawe utaisimamisha hiyo maskani sawasawa na mfano wake uliooneshwa mlimani.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Hivyo utalitengeneza hema hilo kulingana na mfano niliokuonesha mlimani.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Hivyo utalitengeneza hema hilo kulingana na mfano niliokuonesha mlimani.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Hivyo utalitengeneza hema hilo kulingana na mfano niliokuonesha mlimani.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

“Simamisha maskani ya Mungu sawasawa na mfano uliooneshwa kule mlimani.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

“Simamisha Hema sawasawa na mfano ulioonyeshwa kule mlimani.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Nawe utaisimamisha hiyo maskani sawasawa na mfano wake uliooneshwa mlimani.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Kutoka 26:30
14 Marejeleo ya Msalaba  

Hayo yote, akasema Daudi, yamenielea kwa maandiko kutoka kwa mkono wa BWANA, naam, kazi zote za mfano huu.


Nawe angalia ya kwamba uvifanye kama mfano wake, uliooneshwa mlimani.


Sawasawa na haya yote nikuoneshayo, mfano wa maskani, na mfano wa samani zake zote, ndivyo mtakavyovifanya.


Na hizo mbao utazifunika dhahabu, na pete zake za kutilia yale mataruma utazifanya za dhahabu; na hayo mataruma utayafunika dhahabu.


Uifanye ya mbao, yenye mvungu ndani yake; kama ulivyooneshwa mlimani, ndivyo watakavyoifanya.


Siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza utaisimamisha hiyo maskani ya hema ya kukutania.


Ndipo wakasafiri Wakohathi wenye kuvichukua vile vitu vitakatifu; na hao wengine wakaisimamisha maskani kabla hawajaja wao.


Na hii ndiyo kazi ya hicho kinara cha taa, ilikuwa ni kazi ya ufuzi wa dhahabu; tangu kitako chake hata maua yake kilikuwa ni kazi ya ufuzi; vile vile kama ule mfano BWANA aliokuwa amemwonesha Musa, ndivyo alivyokifanya kinara.


Ile hema ya ushahidi ilikuwa pamoja na baba zetu jangwani, kama alivyoagiza yeye aliyesema na Musa, ya kwamba aifanye kulingana na mfano ule aliouona;


mhudumu wa patakatifu, na wa ile hema ya kweli, ambayo Bwana aliiweka wala si mwanadamu.


watumikiao mfano na kivuli cha mambo ya mbinguni, kama Musa alivyoagizwa na Mungu, alipokuwa tayari kuifanya ile hema; maana asema, Angalia ukavifanye vitu vyote kwa mfano ule uliooneshwa katika mlima.


Basi ilikuwa sharti nakala za mambo yaliyo mbinguni zisafishwe kwa hizo, lakini mambo ya mbinguni yenyewe yasafishwe kwa dhabihu zilizo bora kuliko hizo.


Kisha mkutano mzima wa wana wa Israeli walikutana pamoja hapo Shilo, wakasimamisha hema ya kukutania huko; nayo nchi ilikuwa imeshindwa mbele zao.