Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Kutoka 23:1 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Usivumishe habari za uongo; usishirikiane na mwovu kwa kuwa shahidi wa uongo.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

“Usitoe habari za uongo. Usishirikiane na mtu mwovu ili kuwa shahidi mbaya.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

“Usitoe habari za uongo. Usishirikiane na mtu mwovu ili kuwa shahidi mbaya.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

“Usitoe habari za uongo. Usishirikiane na mtu mwovu ili kuwa shahidi mbaya.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

“Usieneze habari za uongo. Usimsaidie mtu mwovu kwa kuwa shahidi mwenye nia ya kudhuru wengine.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

“Usieneze habari za uongo. Usimsaidie mtu mwovu kwa kuwa shahidi mwenye nia ya kudhuru wengine.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Usivumishe habari za uongo; usishirikiane na mwovu kwa kuwa shahidi wa uongo.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Kutoka 23:1
40 Marejeleo ya Msalaba  

Naye akamwambia maneno yayo hayo, akisema, Yule mtumwa Mwebrania uliyemleta kwetu, aliingia kwangu anidhihaki.


Mfalme akasema, Na mwana wa bwana wako yuko wapi? Siba akamwambia mfalme, Angalia, anakaa Yerusalemu; kwani alisema, Leo nyumba ya Israeli watanirudishia ufalme wa babu yangu.


Naye amenisingizia mimi mtumishi wako kwa bwana wangu mfalme; lakini bwana wangu mfalme ni kama malaika wa Mungu; utende basi yaliyo mema machoni pako.


Amsingiziaye jirani yake kwa siri, Huyo nitamwangamiza. Mwenye macho ya kiburi na moyo wa majivuno, Huyo sitamvumilia.


Akupe nini, akuzidishie nini, Ewe ulimi wenye hila?


Asiyesingizia kwa ulimi wake. Wala kumtenda mwenziwe mabaya, Wala kumsengenya jirani yake.


Usinitie katika nia ya watesi wangu; Maana mashahidi wa uongo wamenijia, Nao watoao jeuri kama pumzi.


Mashahidi wa udhalimu wanasimama, Wananiuliza mambo nisiyoyajua.


Usimshuhudie jirani yako uongo.


Jitenge mbali na neno la uongo; wala wasio hatia na wenye haki usiwaue; kwa kuwa mimi sitamhesabia haki yeye aliye mwovu.


Yeye afichaye chuki ana midomo ya uongo, Na yeye asingiziaye ni mpumbavu.


Atamkaye maneno ya kweli hufunua haki; Bali shahidi wa uongo hutamka hila.


Shahidi mwaminifu hatasema uongo; Bali shahidi wa uongo, pumzi zake ni uongo.


Mtenda mabaya husikiliza midomo ya uovu; Na mwongo hutega sikio lake kusikiliza ulimi wa madhara.


Shahidi asiyefaa kitu hudhihaki hukumu, Na vinywa vya wasio haki humeza uovu.


Shahidi wa uongo hakosi ataadhibiwa; Wala asemaye uongo hataokoka.


Shahidi wa uongo hakosi ataadhibiwa; Naye asemaye uongo ataangamia.


Shahidi wa uongo atapotea; Bali mtu asikiaye atasema maneno yadumuyo.


Usimshuhudie jirani yako pasipo sababu, Wala usidanganye kwa midomo yako.


Mtu amshuhudiaye jirani yake uongo Ni nyundo, na upanga, na mshale mkali.


Upepo wa kusi huleta mvua; Vile vile asingiziaye huleta uso wa ghadhabu.


Shahidi wa uongo asemaye uongo; Naye apandaye mbegu za fitina kati ya ndugu.


Maana nimesikia shutuma za watu wengi; hofu ziko pande zote. Rafiki zangu wote, wanaonivizia nisite, husema, Mshitaki, nasi tutamshitaki, huenda akahadaika, nasi tutamshinda, tutajilipiza kisasi kwake.


Msiibe, wala msidanganye, wala msiambiane uongo.


Usiende huku na huko katikati ya watu wako, kama mchongezi; wala usijifaidi kwa damu ya jirani yako; mimi ndimi BWANA.


Akamwambia, Zipi? Yesu akasema, Ni hizi, Usiue, Usizini, Usiibe, Usishuhudie uongo,


Zakayo akasimama, akamwambia Bwana, Tazama, Bwana, nusu ya mali yangu nawapa maskini, na ikiwa nimenyang'anya mtu kitu kwa hila namrudishia mara nne.


Askari nao wakamwuliza, wakisema, Sisi nasi tufanye nini? Akawaambia, Msidhulumu mtu, wala msishitaki kwa uongo; tena mtosheke na mishahara yenu.


Je! Torati yetu humhukumu mtu kabla ya kumsikia kwanza, na kujua atendavyo?


Kwa nini tusiseme (kama tulivyosingiziwa, na kama wengine wanavyokaza kusema ya kwamba twasema hivyo), Na tufanye mabaya, ili yaje mema? Ambao kuhukumiwa kwao kuna haki.


Basi uvueni uongo, mkaseme kweli kila mtu na jirani yake; kwa maana tu viungo, kila mmoja kiungo cha wenzake.


Wala usimshuhudie jirani yako uongo.


wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema,


Nanyi muwe na dhamiri njema, ili katika neno lile mnalosingiziwa, watahayarishwe wale wautukanao mwenendo wenu mwema katika Kristo.


Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye awashitakiye mbele za Mungu wetu, mchana na usiku.