Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Kutoka 18:24 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Basi Musa akasikiza neno la mkwewe, akayafanya yote aliyokuwa amemwambia.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mose alilisikiliza shauri hilo la mkwewe na kufanya kama alivyoshauriwa.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mose alilisikiliza shauri hilo la mkwewe na kufanya kama alivyoshauriwa.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mose alilisikiliza shauri hilo la mkwewe na kufanya kama alivyoshauriwa.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Musa akamsikiliza baba mkwe wake na kufanya kila kitu alichosema.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Musa akamsikiliza baba mkwe wake na kufanya kila kitu alichosema.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Basi Musa akalisikiliza neno la mkwewe, akayafanya yote aliyokuwa amemwambia.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Kutoka 18:24
10 Marejeleo ya Msalaba  

Hata Shekania, mwana wa Yehieli, mmoja wa wazawa wa Elamu, akajibu, akamwambia Ezra, Sisi tumemkosea Mungu wetu, nasi tumeoa wanawake wageni wa watu wa nchi hizi; lakini bado kuna tumaini kwa Israeli katika jambo hili.


Ndipo Ezra akaondoka, akawaapisha wakuu wa makuhani, na Walawi, na Waisraeli wote, ya kwamba watafanya hivyo. Basi wakaapa.


Hao akawachukua salama wala hawakuogopa, Bali bahari iliwafunika adui zao.


Sikiza sasa neno langu, nitakupa shauri, na Mungu na awe pamoja nawe; uwe wewe kwa ajili ya watu mbele ya Mungu, nawe umletee Mungu maneno yao;


Kwamba utafanya jambo hili, na Mungu akikuagiza hivyo, basi utaweza kusimama wewe, na watu hawa wote nao watakwenda mahali pao kwa amani.


Musa akawachagua watu wenye uwezo katika Israeli yote, akawaweka wawe vichwa juu ya watu, wakuu wa maelfu, na wakuu wa mamia, na wakuu wa hamsini hamsini, na wakuu wa kumi kumi.


mwenye hekima asikie na kuongezewa elimu, na mwenye ufahamu ayafikie mashauri yenye njia.


Na jicho haliwezi kuuambia mkono, Sina haja na wewe; wala tena kichwa hakiwezi kuiambia miguu, Sina haja na ninyi.


Nami wakati ule niliwaambia, nikasema, Mimi siwezi kuwachukua peke yangu.