Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Kutoka 17:2 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Kwa hiyo hao watu wakamgombeza Musa, wakasema, Tupe maji tunywe. Musa akawaambia, Kwa nini mnanigombeza? Mbona mnamjaribu BWANA?

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Kwa hiyo watu wakamnungunikia Mose wakisema, “Tupe maji ya kunywa.” Mose akawauliza, “Mbona mnaninungunikia? Mbona mnamjaribu Mwenyezi-Mungu?”

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Kwa hiyo watu wakamnungunikia Mose wakisema, “Tupe maji ya kunywa.” Mose akawauliza, “Mbona mnaninungunikia? Mbona mnamjaribu Mwenyezi-Mungu?”

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Kwa hiyo watu wakamnung'unikia Mose wakisema, “Tupe maji ya kunywa.” Mose akawauliza, “Mbona mnaninung'unikia? Mbona mnamjaribu Mwenyezi-Mungu?”

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Kwa hiyo wakagombana na Musa wakisema, “Tupe maji ya kunywa.” Musa akajibu, “Mbona mnagombana nami? Kwa nini mnamjaribu Mwenyezi Mungu?”

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Kwa hiyo wakagombana na Musa wakisema, “Tupe maji ya kunywa.” Musa akajibu, “Mbona mnagombana nami? Kwa nini mnamjaribu bwana?”

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Kwa hiyo hao watu wakamnung'unikia Musa, wakasema, Tupe maji tunywe. Musa akawaambia, Kwa nini mnaninung'unikia? Mbona mnamjaribu BWANA?

Tazama sura
Tafsiri zingine



Kutoka 17:2
32 Marejeleo ya Msalaba  

Lakini punde wakayasahau matendo yake, Wakakosa kungojea ushauri wake.


Bali walitamani sana nyikani, Wakamjaribu Mungu jangwani.


Wakamjaribu Mungu mioyoni mwao Kwa kutaka chakula kwa tamaa zao.


Wakamjaribu Mungu tena na tena; Na kumkasirisha Mtakatifu wa Israeli.


Lakini walimjaribu Mungu Aliye Juu, wakamwasi, Wala hawakuzishika shuhuda zake.


Msifanye mioyo yenu kuwa migumu; Kama ilivyokuwa huko Meriba Kama siku ile katika Masa jangwani.


Hapo waliponijaribu baba zenu, Wakanipima, wakayaona matendo yangu.


Ndipo watu wakamnung'unikia Musa, wakisema, Tunywe nini?


Musa akasema, Ndilo litakalokuwa, hapo BWANA atakapowapa nyama wakati wa jioni mle, na asubuhi mikate hata mkakinai; kwa kuwa BWANA asikia manung'uniko yenu mliyomnung'unikia yeye; na sisi tu nani? Manung'uniko yenu hayakuwa juu yetu sisi, ila juu ya BWANA.


Akapaita mahali pale jina lake Masa, na Meriba kwa sababu ya ugomvi wa wana wa Israeli, na kwa sababu walimjaribu BWANA, wakisema, Je! BWANA yu kati yetu au sivyo?


wakawaambia, BWANA awaangalie na kuamua; kwa kuwa mmefanya harufu yetu kuwa chukizo mbele ya Farao, na mbele ya watumishi wake, mkatia upanga mikononi mwao, watuue.


Lakini Ahazi akasema, Sitaitaka, wala sitamjaribu BWANA.


Na sasa twasema ya kwamba wenye kiburi ndio walio heri; naam, watendao uovu ndio wajengwao; naam, wamjaribuo Mungu ndio waponywao.


Kisha wana wa Israeli wote wakamnung'unikia Musa na Haruni; mkutano wote wakawaambia, Ingekuwa heri kama tungalikufa katika nchi ya Misri, au, ingekuwa heri kama tungalikufa katika jangwa hili.


kwa sababu watu hawa wote, ambao wameuona utukufu wangu na ishara zangu, nilizozitenda huko Misri, na huko jangwani, pamoja na haya wamenijaribu mara hizi kumi, wala hawakuisikiza sauti yangu;


Watu wakamnung'unikia Mungu, na Musa, Mbona mmetupandisha huku kutoka nchi ya Misri, ili tufe jangwani? Maana hapana chakula, wala hapana maji, na roho zetu zinakinai chakula hiki dhaifu.


Yesu akamwambia, Tena imeandikwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako.


yule mdogo akamwambia babaye, Baba, nipe sehemu ya mali iliyo uridhi wangu. Akawagawia mali yake.


Yesu akajibu akamwambia, Imenenwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako.


Basi sasa mbona mnamjaribu Mungu na kuweka kongwa juu ya shingo za wanafunzi, ambalo baba zetu wala sisi hatukuweza kulibeba.


Petro akamwambia, Imekuwaje hata mkapatana kumjaribu Roho wa Bwana? Angalia, miguu yao waliomzika mumeo ipo mlangoni, nao watakuchukua nje wewe nawe.


Wala tusimjaribu Bwana, kama wengine wao walivyomjaribu, wakauawa na nyoka.


Msimjaribu BWANA, Mungu wenu, kama mlivyomjaribu huko Masa.


Tena huko Tabera, na Masa, na Kibroth-hataava mlimtia BWANA hasira.


Hapo baba zenu waliponijaribu, wakanipima, Wakaona matendo yangu miaka arubaini.


Lakini neno hilo likawa baya machoni pa Samweli, waliposema, Tupe mfalme atuamue. Naye Samweli akamwomba BWANA.