Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Kutoka 16:14 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Na ulipokauka ule umande uliokuwa juu ya nchi, kumbe! Juu ya uso wa bara kitu kidogo kilichoviringana, kidogo kama barafu juu ya nchi.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Umande huo ulipotoweka, kukabaki huko nyikani kitu kama mkate mwembamba na mwepesi.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Umande huo ulipotoweka, kukabaki huko nyikani kitu kama mkate mwembamba na mwepesi.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Umande huo ulipotoweka, kukabaki huko nyikani kitu kama mkate mwembamba na mwepesi.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Umande ulipoondoka, vipande vidogo vidogo kama theluji vilionekana juu ya mchanga wa jangwa.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Wakati umande ulipoondoka, vipande vidogo vidogo kama theluji vilionekana juu ya uso wa jangwa.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Na ulipokauka ule umande uliokuwa juu ya nchi, kumbe! Juu ya uso wa bara kitu kidogo kilichoviringana, kidogo kama barafu juu ya nchi.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Kutoka 16:14
7 Marejeleo ya Msalaba  

Ukawapa chakula toka mbinguni, kwa ajili ya njaa yao, na kwa ajili yao ukaleta maji kutoka mwambani, kwa sababu ya kiu yao, ukawaamuru waingie na kuimiliki, nchi ambayo umeinua mkono wako kuwapa.


Walimwomba naye akaleta kware, Na kuwashibisha chakula cha mbinguni.


Ndiye atoaye theluji kama sufu, Huimwaga barafu yake kama majivu,


Akawanyeshea mana ili wale; Akawapa nafaka ya mbinguni.


Na nyumba ya Israeli wakakiita jina lake Mana; nacho kilikuwa mfano wa chembe za mtama, nyeupe; na utamu wake ulikuwa kama utamu wa maandazi membamba yaliyoandaliwa kwa asali.


Akakunyenyekeza, akakuacha uone njaa, akakulisha kwa mana, usiyoijua wewe wala baba zako hawakuijua; apate kukujulisha ya kuwa mwanadamu haishi kwa mkate tu, bali huishi kwa kila litokalo katika kinywa cha BWANA.