Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Kumbukumbu la Torati 32:29 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Laiti wangekuwa na akili, hata wakafahamu haya, Ili watafakari mwisho wao.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Wangekuwa na hekima wangejua kwa nini walishindwa, wangeweza kuelewa mwisho wao utakuwaje.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Wangekuwa na hekima wangejua kwa nini walishindwa, wangeweza kuelewa mwisho wao utakuwaje.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Wangekuwa na hekima wangejua kwa nini walishindwa, wangeweza kuelewa mwisho wao utakuwaje.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Laiti wangekuwa na hekima wangefahamu hili, na kutambua mwisho wao utakuwaje!

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Laiti wangekuwa na hekima wangefahamu hili, na kutambua mwisho wao utakuwa aje!

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Laiti wangekuwa na akili, hata wakafahamu haya, Ili watafakari mwisho wao.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Kumbukumbu la Torati 32:29
18 Marejeleo ya Msalaba  

Na wamshukuru BWANA kwa fadhili zake, Na maajabu yake kwa wanadamu.


Aliye na hekima na ayaangalie hayo; Na wazitafakari fadhili za BWANA.


Laiti watu wangu wangenisikiliza, Na Israeli angeenenda katika njia zangu;


Basi, utufundishe kuzihesabu siku zetu, Tujipatie moyo wa hekima.


Nanyi mtafanya nini siku ya kujiliwa, na wakati wa uangamivu, utakaokuja kutoka mbali sana? Je! Mtamkimbilia nani mpate msaada? Na utukufu wenu mtauacha wapi?


Ni nani miongoni mwenu atakayetega sikio lake kuyasikia hayo? Atakayesikiliza na kusikia kwa wakati ujao?


Ukasema, Mimi nitakuwa malkia milele; hata hukuyatia hayo moyoni mwako, wala hukukumbuka mwisho wa mambo hayo.


Kama kware akusanyaye makinda asiyoyaangua, ndivyo alivyo mtu ajipatiaye mali, wala si kwa haki, katikati ya maisha yake itamtoka, na mwisho wake atakuwa mpumbavu.


Manabii wanatabiri uongo, na makuhani wanatawala kwa msaada wa hao; na watu wangu wanapenda mambo yawe hivyo. Nanyi mtafanya nini mwisho wake?


Uchafu wake ulikuwa katika marinda yake; Hakukumbuka mwisho wake; Kwa hiyo ameshuka kwa ajabu; Yeye hana mtu wa kumfariji; Tazama, BWANA, mateso yangu; Maana huyo adui amejitukuza.


Ni nani aliye na hekima, naye atayafahamu mambo haya? Ni nani aliye na busara, naye atayajua? Kwa maana njia za BWANA zimenyoka, nao wenye haki watakwenda katika njia hizo; bali waasio wataanguka ndani yake.


Tafakarini, nawaomba; tangu siku hii ya leo na siku zijazo; tangu siku ya ishirini na nne ya mwezi wa tisa, naam, tangu siku hiyo ulipowekwa msingi wa hekalu la BWANA tafakarini haya.


Lakini Mungu akamwambia, Mpumbavu wewe, usiku huu wa leo wanataka roho yako! Na vitu ulivyojiwekea tayari vitakuwa vya nani?


Kwa sababu najua baada ya kufa kwangu mtajiharibu kabisa, na kukengeuka katika njia niliyowaamuru; nayo mabaya yatawapata siku za mwisho, kwa vile mtakavyofanya maovu machoni pa BWANA kumtia kasirani kwa kazi ya mikono yenu.


Laiti wangekuwa na moyo kama huu ndani yao sikuzote, wa kunicha, na kushika amri zangu zote sikuzote, wapate kufanikiwa wao na watoto wao milele!