Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Kumbukumbu la Torati 32:23 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Nitaweka madhara juu yao chungu chungu; Nitawapiga kwa mishale yangu hata ikaishe;

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Nitarundika maafa chungu nzima juu yao, nitawamalizia mishale yangu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Nitarundika maafa chungu nzima juu yao, nitawamalizia mishale yangu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Nitarundika maafa chungu nzima juu yao, nitawamalizia mishale yangu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

“Nitalundika majanga juu yao na kutumia mishale yangu dhidi yao.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

“Nitalundika majanga juu yao na kutumia mishale yangu dhidi yao.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Nitaweka madhara juu yao chungu chungu; Nitawapiga kwa mishale yangu hata ikaishe;

Tazama sura
Tafsiri zingine



Kumbukumbu la Torati 32:23
19 Marejeleo ya Msalaba  

Akapiga mishale, akawatawanya; Umeme, naye akawatimua.


kwa sababu wameniacha mimi, wameifukizia uvumba miungu mingine, ili wapate kunikasirisha kwa kazi yote ya mikono yao; kwa hiyo hasira yangu itawaka juu ya mahali hapa, isizimike.


Akaipiga mishale yake akawatawanya, Naam, umeme mwingi sana, akawatapanya.


Mishale yako ni mikali, katika mioyo ya adui za mfalme; Watu huanguka chini yako.


Tazama, huyu ametunga uovu, Amechukua mimba ya madhara, amezaa uongo.


Umeliongeza hilo taifa, BWANA, umeliongeza taifa; wewe umetukuzwa, umeipanua mipaka yote ya nchi hii.


Amenichoma viuno Kwa mishale ya podo lake.


Maana Bwana MUNGU asema hivi; Je! U zaidi sana nitakapoleta hukumu zangu nne zilizo kali juu ya Yerusalemu, yaani, upanga, na njaa, na wanyama wabaya, na tauni, niwakatilie mbali nayo wanadamu na wanyama?


hapo nitakapoiachilia mishale mibaya ya njaa juu yao, mishale iletayo uharibifu nitakayoiachilia ili kuwaharibu ninyi; nami nitaiongeza njaa juu yenu, na tegemeo lenu la mkate nitalivunja.


Waueni kabisa, wazee, na viijana, na wasichana, na watoto wachanga, na wanawake; lakini msimkaribie mtu yeyote mwenye hiyo alama; tena anzeni katika patakatifu pangu. Basi, wakaanza kwa wazee waliokuwa mbele ya nyumba.


Tena ikiwa baada ya hayo hamtaki kunisikiza, ndipo nitawaadhibu zaidi mara saba kwa ajili ya dhambi zenu.


nami nitawapiga, mara saba kwa ajili ya dhambi zenu.


Lakini itakuwa usipotaka kuisikiza sauti ya BWANA, Mungu wako, usiyaangalie kufanya maagizo yake yote na amri zake, nikuagizazo hivi leo, ndipo zitakapokujia laana hizi zote na kukupata.


BWANA atamtenga kwa uovu, kutoka kabila zote za Israeli, kwa laana zote za agano lililoandikwa katika kitabu hiki cha torati.


Nitailevya mishale yangu kwa damu, Na upanga wangu utakula nyama; Pamoja na damu ya waliouawa na waliotekwa nyara, Katika vichwa vya wakuu wa adui.