Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Isaya 63:17 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Ee BWANA, mbona umetukosesha njia zako, ukatufanya kuwa na mioyo migumu hata tusikuogope? Urudi kwa ajili ya watumishi wako, makabila ya urithi wako.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Ee Mwenyezi-Mungu, mbona unatukosesha njia zako? Mbona unatufanya kuwa wakaidi hata tusikuogope? Rudi ee Mungu kwa ajili ya watumishi wako, makabila ambayo daima yalikuwa mali yako.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Ee Mwenyezi-Mungu, mbona unatukosesha njia zako? Mbona unatufanya kuwa wakaidi hata tusikuogope? Rudi ee Mungu kwa ajili ya watumishi wako, makabila ambayo daima yalikuwa mali yako.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Ee Mwenyezi-Mungu, mbona unatukosesha njia zako? Mbona unatufanya kuwa wakaidi hata tusikuogope? Rudi ee Mungu kwa ajili ya watumishi wako, makabila ambayo daima yalikuwa mali yako.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Ee Mwenyezi Mungu, kwa nini unatuacha twende mbali na njia zako, na kuifanya mioyo yetu migumu hata hatukukuheshimu? Rudi kwa ajili ya watumishi wako, yale makabila ambayo ni urithi wako.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Ee bwana, kwa nini unatuacha twende mbali na njia zako, na kuifanya mioyo yetu migumu hata hatukukuheshimu? Rudi kwa ajili ya watumishi wako, yale makabila ambayo ni urithi wako.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Ee BWANA, mbona umetukosesha njia zako, ukatufanya kuwa na mioyo migumu hata tusikuogope? Urudi kwa ajili ya watumishi wako, makabila ya urithi wako.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Isaya 63:17
23 Marejeleo ya Msalaba  

Kwa moyo wangu wote nimekutafuta, Usiniache nipotee mbali na maagizo yako.


Unielekeze moyo wangu katika shuhuda zako, Wala usiielekee tamaa.


Usiuelekeze moyo wangu kunako jambo baya, Nisiyazoelee matendo yasiyofaa, Pamoja na watu watendao maovu; Wala nisile vyakula vyao vya anasa.


Ee Mungu wa majeshi, tunakusihi, urudi, Utazame toka juu uone, uujie mzabibu huu.


Urudi, Ee BWANA utakasirika hadi lini? Wahurumie watumishi wako.


Musa na Haruni walifanya ajabu hizo zote mbele ya Farao; BWANA akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, asiwape wana wa Israeli ruhusa watoke nchi yake.


BWANA akamwambia Musa, Hapo utakaporudi Misri, angalia ukazifanye mbele ya Farao zile ajabu zote nilizozitia mkononi mwako; lakini nitaufanya mgumu moyo wake, naye hatawapa ruhusa hao watu waende zao.


kwa kuwa BWANA wa majeshi amewabariki, akisema, Wabarikiwe watu wangu Misri; na wewe Ashuru, kazi ya mikono yangu; na wewe Israeli, urithi wangu.


Bwana akanena, Kwa kuwa watu hawa hunikaribia na kuniheshimu kwa vinywa vyao, bali mioyo yao wamefarakana nami, na kicho chao walichonacho kwangu ni maagizo ya wanadamu waliyofundishwa;


kwa sababu hiyo mimi nitafanya tena kazi ya ajabu kati ya watu hawa, kazi ya ajabu na mwujiza; na akili za watu wao wenye akili zitapotea, na ufahamu wa wenye busara wao utafichwa.


na pumzi yake ni kijito kifurikacho, kifikacho hata shingoni, kupepeta mataifa kwa ungo wa ubatili; na lijamu ikoseshayo itakuwa katika taya za watu.


Zifanye akili za watu hawa zipumbae, na uyatie uzito masikio yao, na uyafumbe macho yao; wasije wakaona kwa macho yao, na kusikia kwa masikio yao, na kufahamu kwa mioyo yao, na kurejea na kuponywa.


Ameziziba njia zangu kwa mawe yaliyochongwa; Ameyapotosha mapito yangu.


nami nikawatia unajisi kwa matoleo yao wenyewe, kwa kuwa walipitisha motoni wote waliofungua tumbo; ili kuwafanya kuwa ukiwa, wakapate kujua ya kuwa mimi ndimi BWANA.


Ndipo yule malaika wa BWANA akajibu, akasema, Ee BWANA wa majeshi, hadi lini utakataa kuurehemu Yerusalemu, na miji ya Yuda uliyoikasirikia miaka hii sabini?


Tena hapo liliposimama, akasema, Ee BWANA, uwarudie maelfu kumi ya maelfu ya Israeli.


Amewapofusha macho, Ameifanya mizito mioyo yao; Wasije wakaona kwa macho yao, Wakafahamu kwa mioyo yao, Wakaongoka, nikawaponya.


Lakini Sihoni mfalme wa Heshboni hakutuacha kupitia kwake; kwa kuwa BWANA, Mungu wako, alifanya roho yake kuwa ngumu, akamtia ukaidi moyoni mwake, apate kumtia mkononi mwako kama alivyo hivi leo.


Kwa kuwa lilikuwa ni la BWANA kuifanya mioyo yao kuwa migumu, hata wakatoka kupigana na Israeli, ili apate kuwaangamiza kabisa, wasihurumiwe lakini apate kuwaangamiza, kama vile BWANA alivyomwamuru Musa.