Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Isaya 62:5 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Maana kama vile kijana amwoavyo mwanamwali, ndivyo wana wako watakavyokuoa wewe; na kama vile bwana arusi amfurahiavyo bibi arusi, ndivyo Mungu wako atakavyokufurahia wewe.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Maana kama kijana mwanamume amwoavyo msichana, ndivyo aliyekujenga atakavyokuwa mume wako. Kama bwana arusi afurahivyo juu ya bibi arusi, ndivyo Mungu atakavyofurahi juu yako.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Maana kama kijana mwanamume amwoavyo msichana, ndivyo aliyekujenga atakavyokuwa mume wako. Kama bwana arusi afurahivyo juu ya bibi arusi, ndivyo Mungu atakavyofurahi juu yako.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Maana kama kijana mwanamume amwoavyo msichana, ndivyo aliyekujenga atakavyokuwa mume wako. Kama bwana arusi afurahivyo juu ya bibi arusi, ndivyo Mungu atakavyofurahi juu yako.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Kama vile kijana aoavyo mwanamwali, ndivyo Mwashi wako atakavyokuoa; kama bwana arusi amfurahiavyo bibi arusi wake, ndivyo Mungu wako atakavyokufurahia wewe.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Kama vile kijana aoavyo mwanamwali, ndivyo wanao watakavyokuoa wewe; kama bwana arusi amfurahiavyo bibi arusi wake, ndivyo Mungu wako atakavyokufurahia wewe.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Maana kama vile kijana amwoavyo mwanamwali, ndivyo wana wako watakavyokuoa wewe; na kama vile bwana harusi amfurahiavyo bibi harusi, ndivyo Mungu wako atakavyokufurahia wewe.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Isaya 62:5
12 Marejeleo ya Msalaba  

Tokeni, enyi binti za Sayuni, Mtazameni Mfalme Sulemani, Amevaa taji alilovikwa na mamaye, Siku ya posa yake, Siku ya furaha ya moyo wake.


Bibi arusi, njoo pamoja nami toka Lebanoni, Pamoja nami toka Lebanoni. Shuka kutoka kilele cha Amana, Kutoka vilele vya Seniri na Hermoni; Kutoka mapangoni mwa simba, Kutoka milimani mwa chui.


Hutaitwa tena Aliyeachwa, wala nchi yako haitaitwa tena, Ukiwa; bali utaitwa Hefziba; na nchi yako Beula; kwa kuwa BWANA anakufurahia, na nchi yako itaolewa.


Nami nitaufurahia Yerusalemu, nitawaonea shangwe watu wangu; sauti ya kulia haitasikika ndani yake tena, wala sauti ya kuomboleza.


Naam, nitafurahi juu yao niwatendee mema, nami nitawapanda katika nchi hii kweli kweli, kwa moyo wangu wote, na kwa roho yangu yote.


Nami nitakuposa uwe wangu wa milele; naam, nitakuposa kwa haki, na kwa hukumu, na kwa ufadhili, na kwa rehema.


Tena itakuwa siku hiyo, mimi nitaitika, asema BWANA; nitaziitikia mbingu, nazo zitaiitikia nchi;


BWANA, Mungu wako, yuko katikati yako shujaa awezaye kuokoa; Atakushangilia kwa furaha kuu, Atakutuliza katika upendo wake, Atakufurahia kwa kuimba.


Na mataifa yote watawaiteni heri; maana mtakuwa nchi ya kupendeza sana, asema BWANA wa majeshi.


tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi katika mkono wa kulia wa kiti cha enzi cha Mungu.