Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Isaya 5:21 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Ole wao walio na hekima katika macho yao wenyewe, na wenye busara katika fikira zao wenyewe!

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Ole wao wanaojiona kuwa wenye hekima ambao wanajiona kuwa wenye akili.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Ole wao wanaojiona kuwa wenye hekima ambao wanajiona kuwa wenye akili.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Ole wao wanaojiona kuwa wenye hekima ambao wanajiona kuwa wenye akili.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Ole wao walio na hekima machoni pao wenyewe, na kujiona wenye akili machoni pao wenyewe.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Ole wao walio na hekima machoni pao wenyewe, na kujiona wenye akili machoni pao wenyewe.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Ole wao walio na hekima katika macho yao wenyewe, na wenye busara katika fikira zao wenyewe!

Tazama sura
Tafsiri zingine



Isaya 5:21
13 Marejeleo ya Msalaba  

Lakini mpumbavu aweza kupata ufahamu, Ingawa mwanadamu huzaliwa kama mtoto wa punda mwitu.


Je! Wamwona mtu mwenye hekima machoni pake mwenyewe? Afadhali kumtumaini mpumbavu kuliko yeye.


Mtu mvivu ni mwenye hekima machoni pake, Kuliko watu saba wawezao kutoa sababu.


Usiwe na hekima machoni pako; Mche BWANA, ukajiepushe na uovu.


Kwa maana amesema, Kwa nguvu za mkono wangu nimetenda jambo hili, na kwa hekima yangu; maana mimi nina busara; nami nimeiondoa mipaka ya watu, nikaziteka akiba zao, nikawaangusha waketio juu ya viti vya enzi kama afanyavyo shujaa.


Ni nani uliyemshutumu na kumtukana? Umeinua sauti yako juu ya nani, na kuinua macho yako juu? Juu ya Mtakatifu wa Israeli.


ndiye awatanguaye wakuu, na kuwabatilisha waamuzi wa dunia.


Maana umeutumainia ubaya wako; umesema, Hapana anionaye; hekima yako, na maarifa yako yamekupotosha, nawe umesema moyoni mwako, Mimi ndiye, wala hapana mwingine zaidi yangu mimi.


Yesu akawaambia, Kama mngekuwa vipofu, msingekuwa na dhambi; lakini kwa kuwa sasa mwasema, Twaona; basi dhambi yenu inakaa.


Wakijinena kuwa wenye hekima walipumbazika;


Kwa maana, ndugu zangu, sipendi msiijue siri hii, ili msijione kuwa wenye akili; ya kwamba kwa sehemu ugumu umewapata Israeli, mpaka utimilifu wa Mataifa uwasili.


Mpatane nia zenu ninyi kwa ninyi. Msinuie yaliyo makuu, lakini mkubali kushughulishwa na mambo manyonge. Msiwe watu wa kujivunia akili.