Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Isaya 41:28 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Na nitazamapo, hapana mtu, hata katika watu hao hapana mshauri mmoja, ambaye, nikimwuliza, aweza kunijibu neno.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Nimeangalia kwa makini sana, lakini simwoni yeyote yule; hamna yeyote kati ya hao miungu awezaye kushauri; nikiuliza hakuna awezaye kunijibu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Nimeangalia kwa makini sana, lakini simwoni yeyote yule; hamna yeyote kati ya hao miungu awezaye kushauri; nikiuliza hakuna awezaye kunijibu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Nimeangalia kwa makini sana, lakini simwoni yeyote yule; hamna yeyote kati ya hao miungu awezaye kushauri; nikiuliza hakuna awezaye kunijibu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Ninatazama, lakini hakuna yeyote: hakuna yeyote miongoni mwao awezaye kutoa shauri, hakuna yeyote wa kutoa jibu wakati ninapowauliza.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Ninatazama, lakini hakuna yeyote: hakuna yeyote miongoni mwao awezaye kutoa shauri, hakuna yeyote wa kutoa jibu wakati ninapowauliza.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Na nitazamapo, hapana mtu, hata katika watu hao hapana mshauri mmoja, ambaye, nikimwuliza, aweza kunijibu neno.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Isaya 41:28
9 Marejeleo ya Msalaba  

Humchukua begani, humchukua, wakamsimamisha mahali pake, akasimama; hataondoka katika mahali pake, naam, mmoja atamwita, lakini hawezi kujibu, wala kumwokoa kutoka kwa taabu yake.


Basi, nilipokuja, mbona hapakuwa na mtu? Nilipoita, mbona hapakuwa na mtu aliyenijibu? Je! Mkono wangu ni mfupi, hata nisiweze kukomboa? Au je! Mimi sina nguvu za kuponya? Tazama, kwa kukemea kwangu naikausha bahari, mito ya maji naifanya kuwa jangwa; samaki wao wanuka kwa sababu hapana maji, nao wafa kwa kiu.


Akaona ya kuwa hapana mtu, akastaajabu kwa kuwa hapana mwombezi; basi, mkono wake mwenyewe ndio uliomletea wokovu; na haki yake ndiyo iliyomsaidia.


Nikatazama, wala hapakuwa na wa kunisaidia; Nikashangaa kwa kuwa hakuna mwenye kutegemeza; Basi, mkono wangu mwenyewe uliniletea wokovu, Ghadhabu yangu ndiyo iliyonitegemeza.


mimi nitawaandikia kuuawa kwa upanga, na ninyi nyote mtainama ili kuchinjwa; kwa sababu nilipoita hamkuitika; niliponena, hamkusikia; bali mlitenda yaliyo mabaya machoni pangu, mlichagua mambo nisiyoyafurahia.


Basi wakaingia wenye hekima wote wa mfalme; lakini hawakuweza kuyasoma yale maandiko, wala kumjulisha mfalme tafsiri yake.