Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Isaya 29:5 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Lakini wingi wa adui zako utakuwa kama mavumbi laini, na wingi wao watishao utakuwa kama makapi yapitayo; naam, itakuwa mara na kwa ghafla.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Kundi la maadui zako litakuwa kama vumbi laini, waliokutendea ukatili watakuwa kama makapi. Hayo yatafanyika ghafla.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Kundi la maadui zako litakuwa kama vumbi laini, waliokutendea ukatili watakuwa kama makapi. Hayo yatafanyika ghafla.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Kundi la maadui zako litakuwa kama vumbi laini, waliokutendea ukatili watakuwa kama makapi. Hayo yatafanyika ghafla.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Lakini adui zako wengi watakuwa kama vumbi laini; makundi ya watu wakatili watakuwa kama makapi yanayopeperushwa. Naam, ghafula, mara moja,

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Lakini adui zako wengi watakuwa kama vumbi laini, kundi la wakatili watakuwa kama makapi yapeperushwayo. Naam, ghafula, mara moja,

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Lakini wingi wa adui zako utakuwa kama mavumbi laini, na wingi wao watishao utakuwa kama makapi yapitayo; naam, itakuwa mara na kwa ghafla.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Isaya 29:5
24 Marejeleo ya Msalaba  

Ili wawe kama mabua makavu mbele ya upepo, Kama makapi yaliyochukuliwa na dhoruba?


Sivyo walivyo wasio haki; Hao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.


Wawe kama makapi mbele ya upepo, Malaika wa BWANA akiwaangusha chini.


Nami nitaadhibu ulimwengu kwa sababu ya ubaya wake, na wenye dhambi kwa sababu ya hatia yao; nami nitaikomesha fahari yao wenye kiburi; nami nitayashusha chini majivuno yao walio wakali;


Kwa hiyo watu walio hodari watakutukuza, Miji ya mataifa yatishayo itakuogopa.


Maana umekuwa ngome ya maskini, Ngome ya mhitaji katika dhiki yake, Mahali pa kukimbilia wakati wa tufani, Na kivuli wakati wa joto; Wakati kishindo cha watu wakatili kilipokuwa, Kama dhoruba ipigayo ukuta.


Kama vile joto katika mahali pakavu Utaushusha mshindo wa wageni; Kama ilivyo joto kwa kivuli cha wingu, Wimbo wa hao watishao utashushwa.


Kwa maana mwenye kutisha ameangamizwa, naye mwenye dharau amekoma, nao wote watazamiao uovu wamekatiliwa mbali;


basi, uovu huu utakuwa kwenu kama mahali palipobomoka, kuanguka patokezapo katika ukuta mrefu, ambapo kuvunjika kwake huja ghafla kwa mara moja.


Basi Wamisri ni wanadamu wala si Mungu, na farasi wao ni nyama wala si roho; na BWANA atakaponyosha mkono wake, yeye asaidiaye atajikwaa, na yeye asaidiwaye ataanguka, nao wataangamia wote pamoja.


Ndipo huyo Mwashuri ataanguka kwa upanga ambao si wa mtu; na upanga usio upanga wa mtu utamwangamiza; naye ataukimbia upanga, na vijana wake watatoa kodi.


Basi malaika wa BWANA alitoka, akaua watu elfu mia moja na themanini na tano katika kituo cha Waashuri, na watu walipoamka asubuhi na mapema, kumbe, hao walikuwa maiti wote pia.


Tazama, mataifa ni kama tone la maji katika ndoo, huhesabiwa kuwa kama mavumbi membamba katika mizani; tazama, yeye huvinyanyua visiwa kama ni kitu kidogo sana.


Tazama, wote walioona hasira juu yako watatahayarika na kufadhaika; watu washindanao nawe watakuwa si kitu, na kuangamia.


Tazama, nitakufanya kuwa chombo kikali kipya cha kupuria, chenye meno; utaifikicha milima, na kuisaga; nawe utafanya vilima kuwa kama makapi.


Utawapepeta, na upepo utawapeperusha; upepo wa kisulisuli utawatawanya; nawe utamfurahia BWANA, utajitukuza katika Mtakatifu wa Israeli.


Kwa sababu hiyo uovu utakupata; wala hutaweza kuuagua; na msiba utakuangukia; hutaweza kuuondoa; na ukiwa usioujua utakupata kwa ghafla.


Mimi nimehubiri mambo ya kale tangu zamani; naam, yalitoka katika kinywa changu, nikayadhihirisha; niliyatenda kwa ghafla, yakatokea.


yeye aletaye uharibifu wa ghafla juu ya wenye nguvu, hata kuiharibu ngome.


Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafla, kama vile uchungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa.