Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Isaya 24:12 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Ndani ya mji umebaki ukiwa, na lango lake limepigwa kwa uharibifu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mji ni magofu matupu; malango yake yamevunjwavunjwa.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mji ni magofu matupu; malango yake yamevunjwavunjwa.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mji ni magofu matupu; malango yake yamevunjwavunjwa.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Mji umeachwa katika uharibifu, lango lake limevunjwa vipande.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Mji umeachwa katika uharibifu, lango lake limevunjwa vipande.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Ndani ya mji umebaki ukiwa, na lango lake limepigwa kwa uharibifu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Isaya 24:12
12 Marejeleo ya Msalaba  

Piga yowe, Ee lango; lia, Ee mji; Ee Ufilisti enyi wote, umeyeyuka kabisa; Maana moshi unakuja toka kaskazini, Wala hakuna atakayechelewa katika majeshi yake.


maana jumba la mfalme litaachwa; mji uliokuwa na watu wengi utakuwa hauna mtu; kilima na mnara utakuwa makao ya wanyama milele, furaha ya punda mwitu, malisho ya makundi ya kondoo;


Lakini mvua ya mawe itanyesha, wakati wa kuangushwa miti ya msituni; na huo mji utadhilika.


Nitakwenda mbele yako, na kupasawazisha mahali palipoparuza; nitavunja vipande vipande milango ya shaba, na kukatakata mapingo ya chuma;


Nami nitafanya Yerusalemu kuwa magofu, Makao ya mbweha; Nami nitaifanya miji ya Yuda kuwa ukiwa, Isikaliwe na mtu awaye yote.


Jinsi mji huu ukaavyo ukiwa, Huo uliokuwa umejaa watu! Jinsi alivyokuwa kama mjane, Yeye aliyekuwa mkuu kati ya mataifa! Binti mfalme kati ya majimbo, Jinsi alivyoshikwa shokoa!


Njia za Sayuni zaomboleza, Kwa kuwa hakuna ajaye kwa sikukuu; Malango yake yote yamekuwa ukiwa, Makuhani wake hupiga kite; Wanawali wake wanahuzunika; Na yeye mwenyewe huona uchungu.


Malango yake yamezama katika nchi; Ameyaharibu makomeo yake na kuyavunja; Mfalme wake na wakuu wake wanakaa Kati ya mataifa wasio na sheria; Naam, manabii wake hawapati maono Yatokayo kwa BWANA.


Kwa ajili ya mlima Sayuni ulio ukiwa, Mbweha hutembea juu yake.


Maana wakazi wa Marothi wanasubiri kwa hamu kupata mema; Lakini maangamizi yameshuka toka kwa BWANA, Yamefika katika lango la Yerusalemu.


Kwa maana majeraha yake hayaponyeki; Maana msiba umeijia hata Yuda, Unalifikia lango la watu wangu, Naam, hata Yerusalemu.


Basi yule mfalme akaghadhibika; akatuma majeshi yake, akawaangamiza wauaji wale, akauteketeza mji wao.