Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Isaya 10:33 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Angalia, Bwana, BWANA wa majeshi, atayakata matawi kwa nguvu za kutisha; nao walio warefu wa kimo watakatwa; na hao walioinuka wataangushwa chini;

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Bwana Mwenyezi-Mungu wa majeshi atakata matawi yake kwa ukatili; miti mirefu itaangushwa chini, walio juu wataaibishwa.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Bwana Mwenyezi-Mungu wa majeshi atakata matawi yake kwa ukatili; miti mirefu itaangushwa chini, walio juu wataaibishwa.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Bwana Mwenyezi-Mungu wa majeshi atakata matawi yake kwa ukatili; miti mirefu itaangushwa chini, walio juu wataaibishwa.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Tazama, Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni, atayakata matawi kwa nguvu kuu. Miti mirefu sana itaangushwa, ile mirefu itashushwa chini.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Tazama, Bwana, bwana Mwenye Nguvu Zote, atayakata matawi kwa nguvu kuu. Miti mirefu sana itaangushwa, ile mirefu itashushwa chini.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Angalia, Bwana, BWANA wa majeshi, atayakata matawi kwa nguvu za kutisha; nao walio warefu wa kimo watakatwa; na hao walioinuka wataangushwa chini;

Tazama sura
Tafsiri zingine



Isaya 10:33
17 Marejeleo ya Msalaba  

Naye BWANA akatuma malaika aliyewakatia mbali wapiganaji vita wote, na majemadari, na makamanda, kambini mwa mfalme wa Ashuru. Basi akarudia nchi yake kwa aibu. Naye alipoingia nyumbani mwa mungu wake, baadhi ya wanawe mwenyewe wakamwangamiza humo kwa upanga.


Maana kabla ya mavuno, maua yaangukapo, na maua yakawa zabibu zianzazo kuiva, ndipo atakapoyakata matawi kwa miundu, na kuviondoa vitawi vilivyopanuka na kuvikata.


Lakini mvua ya mawe itanyesha, wakati wa kuangushwa miti ya msituni; na huo mji utadhilika.


Makabila ya watu wamekimbia wakisikia kelele za fujo; mataifa wametawanyika ulipojiinua nafsi yako.


Ikawa alipokuwa akiabudu katika nyumba ya Nisroki, mungu wake, Adrameleki na Shareza, wanawe, wakampiga kwa upanga; wakakimbilia nchi ya Ararati; naye Esar-hadoni, mwanawe, akatawala baada yake.


Na mtu mnyonge ainamishwa, na mtu mkubwa amedhilika, na macho yao walioinuka hunyenyekezwa,


Nami nitawatayarisha waangamizi juu yako, kila mtu na silaha zake; Nao watakata mierezi yako miteule, na kuitupa motoni.


Tazama, Mwashuri alikuwa mwerezi katika Lebanoni, wenye matawi mazuri, na kifuniko chenye uvuli, na kimo kirefu; na kilele chake kilikuwa kati ya matawi mapana.


Basi mimi, Nebukadneza, namhimidi Mfalme wa mbinguni, namtukuza na kumheshimu; maana matendo yake yote ni kweli, na njia zake ni za adili; na wale waendao kwa kutakabari, yeye aweza kuwadhili.


Lakini nilimwangamiza Mwamori mbele yao, ambaye urefu wake ulikuwa kama urefu wa mierezi, tena alikuwa na nguvu kama mialoni; lakini niliyaangamiza matunda yake toka juu, na mizizi yake toka chini.


BWANA asema hivi, Ijapokuwa wana nguvu zilizo timilifu, ijapokuwa ni wengi, hata hivyo watakatwa, naye atapita na kwenda zake. Ingawa nimekutesa, sitakutesa tena.


Kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.