Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Hosea 13:5 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Mimi nilikujua katika jangwa, katika nchi yenye ukame.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Ni mimi niliyewatunza mlipokuwa jangwani, katika nchi iliyokuwa ya ukame.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Ni mimi niliyewatunza mlipokuwa jangwani, katika nchi iliyokuwa ya ukame.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Ni mimi niliyewatunza mlipokuwa jangwani, katika nchi iliyokuwa ya ukame.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Niliwatunza huko jangwani, katika nchi yenye joto liunguzalo.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Niliwatunza huko jangwani, katika nchi yenye joto liunguzalo.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Mimi nilikujua katika jangwa, katika nchi yenye ukame.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Hosea 13:5
16 Marejeleo ya Msalaba  

Hii ilikuwa hali yangu; mchana jua likanipata, na baridi usiku, usingizi ukanitoka machoni mwangu.


Kwa kuwa BWANA anaijua njia ya wenye haki, Bali njia ya wasio haki itapotea.


Roho yangu inapozimia unayajua mapito yangu; Katika njia niendayo wamenifichia mtego.


Na nishangilie, nizifurahie fadhili zako, Kwa kuwa umeyaona mateso yangu. Umeijua nafsi yangu taabuni,


Ee MUNGU, Mungu wangu, nitakutafuta mapema, Nafsi yangu inakuonea kiu, Mwili wangu wakuonea shauku, Katika nchi kame na uchovu, isiyo na maji.


Mungu akawaona wana wa Israeli, na Mungu akawaangalia.


Nenda ukalie masikioni mwa Yerusalemu, ukisema, BWANA asema hivi, Nakukumbuka, hisani ya ujana wako, upendo wa wakati wa kuposwa kwako; Jinsi ulivyonifuata huko jangwani, katika nchi isiyopandwa mbegu.


Wala hawakusema, Yuko wapi BWANA, aliyetutoa katika nchi ya Misri; akatuongoza jangwani, katika nchi ya ukame na mashimo, katika nchi ya kiu na ya kivuli cha mauti, katika nchi ambayo ndani yake hapiti mtu, wala haikukaliwa na watu?


Mimi namjua Efraimu, wala Israeli hakufichwa nisimwone; maana sasa, Ee Efraimu, umefanya uzinzi; Israeli ametiwa unajisi.


Mimi nilimkuta Israeli kama zabibu nyikani; nami niliwaona baba zenu kama matunda ya mtini yaliyoiva kwanza, msimu wake wa kwanza; lakini walikwenda Baal-Peori, wakajiweka wakfu kwa kitu cha aibu, wakawa chukizo kama kitu kile walichokipenda.


BWANA ni mwema, ni ngome siku ya taabu; naye huwajua hao wamkimbiliao.


Lakini mtu akimpenda Mungu, huyo amejulikana naye.


Bali sasa mkiisha kumjua Mungu, au zaidi kujulikana na Mungu, kwa nini kuyarejea tena mafundisho ya kwanza yaliyo manyonge, yenye upungufu, ambayo mnataka kuyatumikia tena?


Kwa kuwa BWANA, Mungu wako, amekubariki katika kazi yote ya mkono wako; amejua ulivyotembea katika jangwa kubwa hili; miaka arubaini hii alikuwa nawe BWANA, Mungu wako; hukukosa kitu.


Alimkuta katika nchi ya ukame, Na katika jangwa tupu litishalo; Alimzunguka, akamtunza; Akamhifadhi kama mboni ya jicho;


aliyekuongoza katika jangwa lile kubwa lenye kitisho, lenye nyoka za moto na nge, nchi ya kiu isiyokuwa na maji; aliyekutolea maji katika mwamba mgumu,