Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Hesabu 9:20 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Na pengine lile wingu lilikaa juu ya maskani siku chache; ndipo kwa amri ya BWANA walikaa katika kambi yao, tena kwa amri ya BWANA walisafiri.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Wakati mwingine wingu hilo lilikaa juu ya hema kwa muda wa siku chache tu; lakini kila wakati Waisraeli walibaki kambini; walihama kama Mwenyezi-Mungu alivyowaamuru.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Wakati mwingine wingu hilo lilikaa juu ya hema kwa muda wa siku chache tu; lakini kila wakati Waisraeli walibaki kambini; walihama kama Mwenyezi-Mungu alivyowaamuru.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Wakati mwingine wingu hilo lilikaa juu ya hema kwa muda wa siku chache tu; lakini kila wakati Waisraeli walibaki kambini; walihama kama Mwenyezi-Mungu alivyowaamuru.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Wakati mwingine wingu lilikuwa juu ya Maskani kwa siku chache tu; kwa amri ya Mwenyezi Mungu wangepiga kambi na kisha kwa amri yake wangeondoka.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Wakati mwingine wingu lilikuwa juu ya Maskani kwa siku chache tu; kwa amri ya bwana wangelipiga kambi na kisha kwa amri yake wangeliondoka.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Na pengine lile wingu lilikaa juu ya maskani siku chache; ndipo kwa amri ya BWANA walikaa katika kambi yao, tena kwa amri ya BWANA walisafiri.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Hesabu 9:20
8 Marejeleo ya Msalaba  

Kwa maana ndivyo alivyo MUNGU, Mungu wetu. Milele na milele Yeye ndiye atakayetuongoza.


Mtumaini BWANA kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe;


Katika njia zako zote mkiri yeye, Naye atayanyosha mapito yako.


Nao wakasafiri kwanza kwa amri ya BWANA kwa mkono wa Musa.


Kwa amri ya BWANA Wana wa Israeli walisafiri, na kwa amri ya BWANA walipiga kambi; wakati lile wingu ilipokaa juu ya maskani walikaa katika kambi yao.


Hata lile wingu lilipokawia juu ya maskani siku nyingi, wana wa Israeli walimtii BWANA, na hawakusafiri.


Na pengine lile wingu lilikaa tangu jioni hata asubuhi; na lile wingu lilipoinuliwa asubuhi walisafiri, au kama likikaa usiku na mchana pia, lilipoinuliwa lile wingu, ndipo waliposafiri.


Usiingiwe na hofu kwa sababu yao; kwa kuwa BWANA, Mungu wako, yuko pamoja nawe, Mungu mkuu, mwenye utisho.