Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Hesabu 16:32 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

nchi ikafunua kinywa chake, na kuwameza, na watu wa nyumba zao na wote walioshikamana na Kora, na vyombo vyao vyote.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

kuwameza watu hao, jamaa zao, pamoja na wafuasi wote wa Kora na mali zao zote.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

kuwameza watu hao, jamaa zao, pamoja na wafuasi wote wa Kora na mali zao zote.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

kuwameza watu hao, jamaa zao, pamoja na wafuasi wote wa Kora na mali zao zote.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

nchi ikafunua kinywa chake na kuwameza wao, pamoja na jamaa zao, na watu wote wa Kora na mali yao yote.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

nchi ikafunua kinywa chake na kuwameza wao, pamoja na jamaa zao, na watu wote wa Kora na mali zao zote.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

nchi ikafunua kinywa chake, na kuwameza, na watu wa nyumba zao na wote walioshikamana na Kora, na vyombo vyao vyote.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Hesabu 16:32
21 Marejeleo ya Msalaba  

Basi sasa, umelaaniwa wewe katika ardhi, iliyofumbua kinywa chake ipokee damu ya ndugu yako kutoka kwa mkono wako;


Wana wa Kohathi; mwanawe huyo ni Ishari, na mwanawe huyo ni Kora, na mwanawe huyo ni Asiri;


mwana wa Tahathi, mwana wa Asiri, mwana wa Ebiasafu, mwana wa Kora;


Nchi ikapasuka ikammeza Dathani, Ikaufunika mkutano wa Abiramu.


Kama kupasua kuni na kuzichanja juu ya nchi, Ndivyo ilivyo mifupa yetu mdomoni pa kuzimu.


Maskani zako zapendeza kama nini, Ee BWANA wa majeshi!


BWANA, umeiridhia nchi yako, Umewarejesha mateka wa Yakobo.


Ee BWANA, Mungu wa wokovu wangu Mchana na usiku nimelia mbele zako.


Dunia kuvunjika, inavunjika sana; dunia kupasuka, imepasuka sana; dunia kutikisika, imetikisika sana.


Kwa hiyo kuzimu kumeongeza tamaa yake, kumefunua kinywa chake bila kiasi; na utukufu wao, na wingi wao, na ghasia yao, naye pia afurahiye miongoni mwao, hushuka na kuingia humo.


mkatwae kila mtu chetezo chake, na kutia uvumba juu yake, mkavilete mbele za BWANA, vyetezo mia mbili na hamsini; wewe pia, na Haruni, kila mtu na awe na chetezo chake.


Lakini BWANA akiumba kitu kipya, na hiyo nchi ikifunua kinywa chake na kuwameza, pamoja na wote walio nao, nao wakashuka shimoni wakiwa hai; ndipo mtatambua ya kwamba watu hawa wamemdharau BWANA


Basi ilikuwa, hapo alipokwisha kusema maneno haya yote, nchi iliyokuwa chini yao ikapasuka;


Basi wao, na wote waliokuwa nao, wakashukia shimoni wakiwa hai; nayo nchi ikawafunika wakaangamia kutoka mle mkutanoni.


Basi waliokufa kwa tauni walikuwa elfu kumi na nne na mia saba, zaidi ya hao waliokufa katika jambo la Kora.


nchi ikafunua kinywa chake, na kuwameza pamoja na Kora, mkutano huo ulipokufa; wakati moto ulipowateketeza watu mia mbili na hamsini, nao wakawa ishara.


Hata hivyo, hao wana wa Kora hawakufa.


Baba yetu alikufa nyikani, naye hakuwamo katika mkutano wa hao waliojikutanisha kinyume cha BWANA katika mkutano wa Kora; lakini akafa katika dhambi zake mwenyewe; naye alikuwa hana wana wa kiume.


Msilitenge kabisa kabila la jamaa za Wakohathi katika hao Walawi;


na alivyowafanya Dathani, na Abiramu, wana wa Eliabu mwana wa Reubeni; nchi ilivyofunua kinywa chake, ikawameza, na walio nyumbani mwao, na mahema yao, na kila kitu kilichokuwa hai kikiwafuata, katikati ya Israeli yote;


Nchi ikamsaidia mwanamke; nchi ikafunua kinywa chake, ikaumeza mto ule lililoutoa lile joka katika kinywa chake.