Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Hesabu 10:35 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Ilikuwa, hapo sanduku liliposafiri kwenda mbele, ndipo Musa akasema, Inuka, Ee BWANA, adui zako na watawanyike; na wakimbie mbele zako hao wakuchukiao.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Kila wakati sanduku liliposafiri kwenda mbele, Mose alisema, “Inuka, ee Mwenyezi-Mungu, uwatawanye adui zako, na hao wanaokuchukia uwafanye wakimbie kutoka mbele yako.”

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Kila wakati sanduku liliposafiri kwenda mbele, Mose alisema, “Inuka, ee Mwenyezi-Mungu, uwatawanye adui zako, na hao wanaokuchukia uwafanye wakimbie kutoka mbele yako.”

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Kila wakati sanduku liliposafiri kwenda mbele, Mose alisema, “Inuka, ee Mwenyezi-Mungu, uwatawanye adui zako, na hao wanaokuchukia uwafanye wakimbie kutoka mbele yako.”

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Wakati wowote Sanduku lilipoondoka, Musa alisema, “Ee Mwenyezi Mungu, inuka! Watesi wako na watawanyike; adui zako na wakimbie mbele zako.”

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Wakati wowote Sanduku lilipoondoka, Musa alisema, “Ee bwana, inuka! Watesi wako na watawanyike; adui zako na wakimbie mbele zako.”

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Ilikuwa, hapo sanduku liliposafiri kwenda mbele, ndipo Musa akasema, Inuka, Ee BWANA, adui zako na watawanyike; na wakimbie mbele zako hao wakuchukiao.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Hesabu 10:35
10 Marejeleo ya Msalaba  

Ee BWANA, uinuke, uende kwenye raha yako, Wewe na sanduku la nguvu zako.


Wokovu ni wa BWANA; Baraka yako na iwe juu ya watu wako.


Inuka, ee BWANA, mwanadamu asipate nguvu, Mataifa wahukumiwe mbele zako.


Ni nani atakayesimama Kwa ajili yangu juu ya wabaya? Ni nani atakayenisaidia Juu yao wafanyao maovu?


Amka, amka, jivike nguvu, Ee mkono wa Bwana; Amka kama katika siku zile za kale, Katika vizazi vile vya zamani.


Nikiunoa upanga wangu wa umeme, Mkono wangu ukishika hukumu, Nitawatoza kisasi adui zangu, Nitawalipa wanaonichukia.


naye huwalipa wamchukiao mbele ya uso wao, kuwaangamiza. Hatakuwa mlegevu kwake yeye amchukiaye, atamlipa mbele ya uso wake.


Hata watu walipofika kambini, wazee wa Israeli wakasema, Mbona BWANA ametupiga leo mbele ya Wafilisti? Twende tukalilete sanduku la Agano la BWANA kutoka Shilo hadi huku, lije kati yetu, na kutuokoa katika mikono ya adui zetu.