Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Ezekieli 23:16 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Na mara alipowaona aliwapendelea, akatuma wajumbe kwao hata Ukaldayo.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Alipoziona picha hizo, mara akashikwa na tamaa, akatuma wajumbe kwenda Ukaldayo.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Alipoziona picha hizo, mara akashikwa na tamaa, akatuma wajumbe kwenda Ukaldayo.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Alipoziona picha hizo, mara akashikwa na tamaa, akatuma wajumbe kwenda Ukaldayo.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Mara tu alipowaona, aliwatamani, akatuma wajumbe kwao huko Ukaldayo.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Mara tu alipowaona, aliwatamani, akatuma wajumbe kwao huko Ukaldayo.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Na mara alipowaona aliwapendelea, akatuma wajumbe kwao hata Ukaldayo.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Ezekieli 23:16
17 Marejeleo ya Msalaba  

Mwanamke alipoona ya kuwa ule mti wafaa kwa chakula, wapendeza macho, nao ni mti wa kutamanika kwa maarifa, basi alichuma matunda yake akala, akampa na mumewe, naye akala.


Ikawa baada ya mambo hayo, mke wa bwana wake akamtamani Yusufu, akamwambia, Lala nami.


wana wa Mungu waliwaona hao binti za wanadamu ya kuwa ni wazuri; wakajitwalia wake wowote waliowachagua.


Ikawa wakati wa jioni, Daudi akaondoka kitandani, akatembea juu ya dari la jumba la mfalme; na alipokuwa juu ya dari aliona mwanamke anaoga; naye huyo mwanamke alikuwa mzuri sana, wa kupendeza macho.


Katika siku zake akakwea Nebukadneza, mfalme wa Babeli, na Yehoyakimu akawa mtumishi wake muda wa miaka mitatu; kisha, akageuka, akamwasi.


Nilifanya agano na macho yangu; Basi ningewezaje kumwangalia msichana?


Unigeuze macho yangu nisitazame visivyofaa, Unihuishe katika njia yako.


Macho yako yataona mambo mageni; Na moyo wako utatoa yaliyopotoka.


Usiutamani uzuri wake moyoni mwako; Wala usikubali akunase kwa kope za macho yake.


Ulimwendea mfalme na mafuta ya marhamu, ukaongeza manukato yako, ukawatuma wajumbe wako waende mbali, ukajidhili sana hadi kuzimu.


Pia ulivitwaa vyombo vyako vya uzuri, vya dhahabu yangu na vya fedha yangu, nilivyokupa, ukajifanyia sanamu za wanaume, ukafanya mambo ya kikahaba pamoja nazo;


Pamoja na hayo umeongeza mambo yako ya kikahaba katika nchi ya Kanaani, mpaka Ukaldayo, wala hujashibishwa kwa hayo.


waliofungiwa mikumbuu viunoni mwao, na vilemba vilivyotiwa rangi vichwani mwao; wote wakuu wa kuangaliwa, kwa mfano wa wana wa Babeli katika Ukaldayo, katika nchi ya kuzaliwa kwao.


Akawapendelea wapenzi wao, ambao nyama ya mwili wao ni kama nyama ya mwili wa punda, nacho kiwatokacho ni kama kiwatokacho farasi.


lakini mimi nawaambia, Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake.


wenye macho yajaayo uzinzi, watu wasiokoma kutenda dhambi, wenye kuhadaa roho zisizo imara, wenye mioyo iliyozoezwa kutamani, wana wa laana;