Waandaa meza mbele yangu, Machoni pa watesi wangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, Na kikombe changu kinafurika.
Ezekieli 16:9 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC Kisha nikakuosha kwa maji; naam, nilikuosha kabisa damu yako, na kukupaka mafuta; Matoleo zaidiBiblia Habari Njema “Kisha nikachukua maji, nikakuosha damu uliyokuwa nayo, nikakupaka mafuta. Biblia Habari Njema - BHND “Kisha nikachukua maji, nikakuosha damu uliyokuwa nayo, nikakupaka mafuta. Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza “Kisha nikachukua maji, nikakuosha damu uliyokuwa nayo, nikakupaka mafuta. Neno: Bibilia Takatifu “ ‘Nilikuogesha kwa maji, nikakuosha ile damu na kukupaka mafuta. Neno: Maandiko Matakatifu “ ‘Nilikuogesha kwa maji, nikakuosha ile damu na kukupaka mafuta. BIBLIA KISWAHILI Kisha nikakuosha kwa maji; naam, nilikuosha kabisa damu yako, na kukupaka mafuta; |
Waandaa meza mbele yangu, Machoni pa watesi wangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, Na kikombe changu kinafurika.
hapo Bwana atakapokuwa ameuosha uchafu wa hao binti za Sayuni na kuisafisha damu ya Yerusalemu kati yake, kwa roho ya hukumu na kwa roho ya kuteketeza.
nikakuvika nguo ya taraza, nikakupa viatu vya ngozi ya pomboo, nikakufunga nguo ya kitani safi kiunoni mwako, nikakufunika kwa hariri.
Na kuhusu habari za kuzaliwa kwako, siku ile uliyozaliwa, kitovu chako hakikukatwa, wala hukuoshwa kwa maji usafishwe; hukutiwa chumvi hata kidogo, wala hukutiwa katika nguo kabisa.
Nami nitawanyunyizia maji safi, nanyi mtakuwa safi; nitawatakaseni kutoka kwa uchafu wenu wote, na kutoka kwa vinyago vyenu vyote.
Na baadhi yenu mlikuwa watu wa namna hii; lakini mlioshwa, lakini mlitakaswa, lakini mlihesabiwa haki katika jina la Bwana Yesu Kristo, na katika Roho wa Mungu wetu.
Nanyi, mafuta yale mliyoyapata kwake yanakaa ndani yenu, wala hamna haja ya mtu kuwafundisha; lakini kama mafuta yake yanavyowafundisha habari za mambo yote, tena ni kweli wala si uongo, na kama yalivyowafundisha, kaeni ndani yake.
Kwa maana wako watatu washuhudiao [mbinguni, Baba, na Neno, na Roho Mtakatifu, na watatu hawa ni umoja.
Basi wewe oga, ujipake mafuta ujivike mavazi yako, kisha uende kwenye uga; lakini usijioneshe kwake mtu yule, ila atakapokwisha kula na kunywa.