Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Ezekieli 14:1 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Ndipo baadhi ya wazee wa Israeli wakanijia, wakaketi mbele yangu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Siku moja baadhi ya wazee wa Israeli walinitembelea kutaka shauri.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Siku moja baadhi ya wazee wa Israeli walinitembelea kutaka shauri.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Siku moja baadhi ya wazee wa Israeli walinitembelea kutaka shauri.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Baadhi ya wazee wa Israeli walinijia na kuketi mbele yangu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Baadhi ya wazee wa Israeli walinijia na kuketi mbele yangu.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Ndipo baadhi ya wazee wa Israeli wakanijia, wakaketi mbele yangu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Ezekieli 14:1
13 Marejeleo ya Msalaba  

Lakini Elisha alikuwa akikaa nyumbani mwake, na wazee wakikaa pamoja naye; na mfalme akamtuma mtu wa mbele yake; lakini hata kabla ya kufika kwake yule aliyetumwa, akawaambia wazee, Je! Mwaona jinsi huyu mwana wa mwuaji alivyotuma aniondolee kichwa changu? Angalieni, huyo aliyetumwa akifika, fungeni mlango, mkamzuie mlangoni; je! Sauti ya miguu ya bwana wake haiko nyuma yake?


Mlinzi akasema, Mchana unakuja na usiku pia; mkitaka kuuliza, ulizeni; njoni tena.


Bwana akanena, Kwa kuwa watu hawa hunikaribia na kuniheshimu kwa vinywa vyao, bali mioyo yao wamefarakana nami, na kicho chao walichonacho kwangu ni maagizo ya wanadamu waliyofundishwa;


Ndipo neno la BWANA likanijia, kusema,


Ikawa katika mwaka wa saba, mwezi wa tano, siku ya kumi ya mwezi, baadhi ya wazee wa Israeli walikuja ili kuuliza kwa BWANA, wakaketi mbele yangu.


Mwanadamu, sema na wazee wa Israeli, uwaambie, Bwana MUNGU asema hivi; Je! Mmekuja kuniuliza neno? Kama mimi niishivyo, asema Bwana MUNGU, sitaulizwa neno na ninyi.


Nao huja kwako kama watu wajavyo, nao hukaa mbele yako kama watu wangu, nao husikia maneno yako, wasiyatende; maana kwa vinywa vyao hujifanya kuwa wenye upendo mwingi, lakini mioyo yao inatafuta faida yao.


Na tazama, wewe umekuwa kwao kama wimbo mzuri sana, wa mtu mwenye sauti ipendezayo, awezaye kupiga kinanda vizuri; maana, wasikia maneno yako, lakini hawayatendi.


Ikawa katika mwaka wa sita, mwezi wa sita, siku ya tano ya mwezi, nilipokuwa nikikaa nyumbani mwangu, wazee wa Yuda nao wakiwa wamekaa mbele yangu, mkono wa Bwana MUNGU ukaniangukia huko.


Naye alikuwa na dada yake aitwaye Mariamu, aliyeketi miguuni pake Yesu, akasikiliza maneno yake.


Mimi ni mtu wa Kiyahudi, nilizaliwa Tarso, mji wa Kilikia, ila nililelewa katika mji huu, miguuni pa Gamalieli, nikafundishwa sheria ya baba zetu kwa usahihi, nikawa mtu wa jitihada kubwa kwa Mungu kama ninyi nyote mlivyo leo hivi;


Kesho yake, wakubwa na wazee na waandishi wakakusanyika Yerusalemu,


Ndipo Petro, akijaa Roho Mtakatifu, akawaambia, Enyi wakubwa wa watu na wazee wa Israeli,