Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Esta 9:16 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Nao Wayahudi wengine waliokaa katika mikoa ya mfalme walikusanyika, wakayapigania maisha yao, wakajipatia raha mbele ya adui zao, wakawaua waliowachukia, watu elfu sabini na tano; lakini juu ya nyara hawakuweka mikono.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Wayahudi waliokuwa katika mikoa nao pia walijiandaa kuyalinda maisha yao. Wakaokolewa kutoka kwa maadui wao; waliwaua watu wapatao 75,000, lakini hawakuchukua nyara.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Wayahudi waliokuwa katika mikoa nao pia walijiandaa kuyalinda maisha yao. Wakaokolewa kutoka kwa maadui wao; waliwaua watu wapatao 75,000, lakini hawakuchukua nyara.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Wayahudi waliokuwa katika mikoa nao pia walijiandaa kuyalinda maisha yao. Wakaokolewa kutoka kwa maadui wao; waliwaua watu wapatao 75,000, lakini hawakuchukua nyara.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Wakati ule ule, Wayahudi wengine waliokuwa kwenye majimbo ya mfalme, wakakusanyika kujilinda nao wakapata nafuu kutokana na adui zao. Waliua adui zao wapatao elfu sabini na tano, lakini hawakugusa nyara zao.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Wakati ule ule, Wayahudi wengine waliokuwa kwenye majimbo ya mfalme, wakakusanyika kujilinda nao wakapata nafuu kutokana na adui zao. Waliua adui zao wapatao 75,000 lakini hawakugusa nyara zao.

Tazama sura

Swahili Roehl Bible 1937

Nao wale Wayuda wengine waliokuwa katika majimbo wakakusanyika, wajisimamie wenyewe na kujiokoa, wajipatie utulivu kwao adui zao, wakaua wachukivu wao 75000, lakini mali zao hawakuziteka kwa mikono yao.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Esta 9:16
6 Marejeleo ya Msalaba  

Wana wa Yakobo wakawajia hao waliouawa, wakaupora mji kwa sababu wamemharibu dada yao.


Katika barua hizo mfalme aliwaruhusu Wayahudi katika kila mji wakusanyike na kuyalinda maisha yao, kwa kuangamiza, kuua, na kulimaliza jeshi lote la watu au mkoa watakaowashambulia, pamoja na watoto na wanawake; na kuyachukua mali yao kuwa nyara;


siku ile ile Wayahudi wakakusanyika mijini mwao katika mikoa yote ya mfalme Ahasuero ili kuwatia mikono wale watu waliowatakia hasara; wala asiweze mtu kuwazuia, kwa kuwa waogopwa na watu wote.


Ili kufanya kisasi juu ya mataifa, Na adhabu juu ya makabila ya watu.


Upanga wao utaingia mioyoni mwao wenyewe, Na nyuta zao zitavunjika.