Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Esta 3:5 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Hata Hamani alipoona ya kwamba Mordekai hamwinamii wala kumsujudia, alighadhibika sana.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Hamani aliwaka hasira alipojua kwamba Mordekai hamwinamii wala hamsujudii.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Hamani aliwaka hasira alipojua kwamba Mordekai hamwinamii wala hamsujudii.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Hamani aliwaka hasira alipojua kwamba Mordekai hamwinamii wala hamsujudii.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Hamani alipoona kuwa Mordekai hampigii magoti wala kumpa heshima, alighadhibika.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Wakati Hamani alipoona kuwa Mordekai hampigii magoti wala kumpa heshima alighadhibika.

Tazama sura

Swahili Roehl Bible 1937

Hamani alipoona, ya kuwa Mordekai hampigii magoti, wala hamwangukii, ndipo, makali yenye moto yalipomjaa Hamani moyoni.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Esta 3:5
13 Marejeleo ya Msalaba  

Bali Vashti, malkia, hakutii amri ya mfalme, alikataa kuja kama alivyoamriwa na mfalme kupitia kwa matowashi; kwa hiyo mfalme akaghadhibika sana, na hasira yake ikawaka ndani yake.


Nao watumishi wote wa mfalme, walioketi langoni pa mfalme, wakainama na kumsujudia Hamani, maana ndivyo mfalme alivyoamuru wamfanyie. Lakini Mordekai hakumwinamia, wala kumsujudia.


Ikawa, waliposema naye kila siku asiwasikilize, wakamwarifu Hamani, ili kuona kama mambo yake Mordekai yatasimama; maana alikuwa amewaambia ya kuwa yeye ni Myahudi.


Basi Hamani alitoka siku ile kwa furaha na ukunjufu wa moyo; lakini Hamani alipomwona Mordekai mlangoni pa mfalme, ya kwamba hasimami wala kunyenyekea mbele yake, alijaa ghadhabu juu ya Mordekai.


Kwani hasira humwua mtu mpumbavu, Nao wivu humwua mjinga.


Asiye haki hunuia mabaya juu ya mwenye haki, Na kumsagia meno yake.


Ghadhabu ya mpumbavu hujulikana mara; Bali mtu mwerevu husitiri aibu.


Mtu wa hasira nyingi atachukua adhabu yake, Maana ujapomwokoa huna budi kufanya tena.


Mwenye kiburi na kutakabari, jina lake ni mbishi; Hutenda mambo katika majivuno ya kiburi chake.


ya kuwa upumbavu huwekwa mahali pa juu sana, nao wakwasi hukaa mahali pa chini.


Ndipo Nebukadneza akajaa ghadhabu, na sura ya uso wake ikabadilika juu ya Shadraka, na Meshaki, na Abednego, basi akatoa amri watie moto ile tanuri mara saba kuliko desturi yake ya kutiwa moto.