Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Esta 3:11 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Kisha mfalme akamwambia Hamani, Hiyo fedha umepewa, na watu pia, fanya uonavyo vema.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Ndipo mfalme akamwambia Hamani, “Umepewa watu wote na hizo fedha, tumia upendavyo.”

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Ndipo mfalme akamwambia Hamani, “Umepewa watu wote na hizo fedha, tumia upendavyo.”

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Ndipo mfalme akamwambia Hamani, “Umepewa watu wote na hizo fedha, tumia upendavyo.”

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Mfalme akamwambia Hamani, “Baki na fedha yako na uwatendee hao watu utakavyo.”

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Mfalme akamwambia Hamani, “Baki na fedha yako na uwatendee hao watu utakavyo.”

Tazama sura

Swahili Roehl Bible 1937

Mfalme akamwambia Hamani: Zile fedha umepewa kukaa nazo, nao watu wa ule ukoo uwafanyizie yaliyo mema machoni pako.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Esta 3:11
6 Marejeleo ya Msalaba  

Ndipo mfalme alipoivua pete yake ya kupigia mhuri kutoka mkononi, akampa Hamani mwana wa Hamedatha, Mwagagi, adui ya Wayahudi.


Basi, waandishi wa mfalme wakaitwa, siku ya kumi na tatu ya mwezi wa kwanza; na barua zikaandikwa, kama vile Hamani alivyoagiza, kwa wakuu wa mfalme, na wakuu wa mikoa, na wakuu wa kila taifa; kila mkoa kwa mwandiko wake, na kila taifa kwa lugha yake; zikaandikwa kwa jina la mfalme Ahasuero, na kutiwa mhuri kwa pete yake.


Macho yao hutokeza kwa kunenepa, Wameipita kadiri ya mawazo ya mioyo yao.


Lakini kwangu mimi, tazama, mimi nipo hapa mikononi mwenu; nitendeni myaonayo kuwa mema na haki mbele ya macho yenu.


Na sasa, tazama, nakufungulia leo minyororo hii iliyo mikononi mwako. Kama ukiona ni vema kwenda Babeli pamoja nami, haya! Njoo, nami nitakutunza sana; lakini kama ukiona ni vibaya kwenda Babeli pamoja nami, basi, acha; tazama, nchi yote iko mbele yako; palipo pema machoni pako na pa kukufaa, nenda huko.


Akamfungua yule aliyetupwa gerezani kwa ajili ya fitina na uuaji, yule waliyemtaka, akamtoa Yesu wamfanyie watakavyo.