Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Esta 1:8 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Walikunywa kama ilivyoamriwa, bila kushurutishwa; maana mfalme aliwaagiza watumishi wahudumie kila mtu kadiri ya mahitaji yake.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Kila mtu alikunywa akashiba; mfalme alikuwa ametoa maagizo kwa watumishi wa ikulu wamhudumie kila mtu kadiri ya mahitaji yake.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Kila mtu alikunywa akashiba; mfalme alikuwa ametoa maagizo kwa watumishi wa ikulu wamhudumie kila mtu kadiri ya mahitaji yake.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Kila mtu alikunywa akashiba; mfalme alikuwa ametoa maagizo kwa watumishi wa ikulu wamhudumie kila mtu kadiri ya mahitaji yake.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Kwa amri ya mfalme kila mgeni aliruhusiwa kunywa alichotaka, kwa kuwa mfalme alitoa maagizo kwa watumishi wote kugawa mvinyo kila mtu kwa jinsi alivyotaka.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Kwa amri ya mfalme kila mgeni aliruhusiwa kunywa alichotaka, kwa kuwa mfalme alitoa maagizo kwa watumishi wote wa kuhudumu mvinyo kumhudumia kila mtu kwa jinsi alivyotaka.

Tazama sura

Swahili Roehl Bible 1937

Kama ilivyoagizwa, watu wakanywa, kama walivyotaka pasipo kushurutishwa; kwani nidvyo, mfalme alivyowaagiza wakuu wote wa nyumbani mwake, waache, kila mtu anywe, kama anavyopendezwa.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Esta 1:8
6 Marejeleo ya Msalaba  

Wakawanywesha kileo katika vyombo mbalimbali vya dhahabu, na divai tele ya kifalme, kufuatana na ukarimu wa ufalme;


Naye Vashti, malkia, akawafanyia karamu wanawake ndani ya nyumba ya kifalme ya mfalme Ahasuero.


Nasi tumeitii sauti ya Yonadabu, mwana wa Rekabu, baba yetu, katika yote aliyotuamuru, kwamba tusinywe divai siku zetu zote, sisi, na wake zetu, na wana wetu, na binti zetu;


Babeli umekuwa kikombe cha dhahabu mkononi mwa BWANA; kilicholevya dunia yote; mataifa wamekunywa mvinyo wake; kwa sababu hiyo mataifa wameingiwa na wazimu.


Akawaambia, Sasa tekeni, mkampelekee mkuu wa sherehe. Wakapeleka.