Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




2 Wafalme 19:25 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Je! Hukusikia wewe ya kuwa mimi ndimi niliyeyatenda hayo tokea zamani, na kuyafanya tokea siku za kale? Sasa mimi nimelitimiza jambo hili, iwe kazi yako kuangamiza miji yenye boma, hata ikawe chungu na magofu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

‘Je, hujasikia, kwamba nilipanga jambo hili tangu awali? Ninachotekeleza sasa nilikipanga zamani.’ Nilikuweka uijenge miji yenye ngome kwa rundo la magofu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

‘Je, hujasikia, kwamba nilipanga jambo hili tangu awali? Ninachotekeleza sasa nilikipanga zamani.’ Nilikuweka uijenge miji yenye ngome kwa rundo la magofu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

‘Je, hujasikia, kwamba nilipanga jambo hili tangu awali? Ninachotekeleza sasa nilikipanga zamani.’ Nilikuweka uijenge miji yenye ngome kwa rundo la magofu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

“ ‘Je, hujasikia? Zamani sana niliamuru hili. Siku za kale nilipanga hili; sasa nimelifanya litokee, kwamba umegeuza miji yenye ngome kuwa malundo ya mawe.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

“ ‘Je, hujasikia? Zamani sana niliamuru hili. Siku za kale nilipanga hili; sasa nimelifanya litokee, kwamba umegeuza miji yenye ngome kuwa malundo ya mawe.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Je! Hukusikia wewe ya kuwa mimi ndimi niliyeyatenda hayo tokea zamani, na kuyafanya tokea siku za kale? Sasa mimi nimelitimiza jambo hili, iwe kazi yako kuangamiza miji yenye boma, hata ikawe chungu na magofu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



2 Wafalme 19:25
11 Marejeleo ya Msalaba  

Shauri la BWANA lasimama milele, Makusudi ya moyo wake vizazi na vizazi.


Maana hasira ya binadamu itakusifu, Masalio ya hasira utajifunga kama mshipi.


Je! Shoka lijisifu juu yake alitumiaye? Je! Msumeno ujitukuze juu yake auvutaye? Ingekuwa kana kwamba bakora ingewatikisa waiinuao, au fimbo ingemwinua yeye ambaye si mti.


Mimi naiumba nuru, na kulihuluku giza; mimi nafanya suluhu, na kuhuluku ubaya; Mimi ni BWANA, niyatendaye hayo yote.


Dondokeni, enyi mbingu, toka juu, Mawingu na yamwage haki; Nchi na ifunuke, ili kutoa wokovu, Nayo itoe haki ikamee pamoja; Mimi, BWANA, nimeiumba.


Tazama, nimemwumba mhunzi afukutaye moto wa makaa, akatoa silaha kwa kazi yake; nami nimemwumba mharibu ili aharibu.


Kwa ajili ya hayo nitafanya Samaria kuwa kama chungu katika shamba, na kama miche ya shamba la mizabibu; nami nitayatupa mawe yake bondeni, nami nitaifunua misingi yake.