Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




2 Samueli 16:20 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Kisha Absalomu akamwambia Ahithofeli, Haya, toa ushauri wako, tufanyeje.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Ndipo Absalomu alipomwambia Ahithofeli, “Nishauri; tufanye nini?”

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Ndipo Absalomu alipomwambia Ahithofeli, “Nishauri; tufanye nini?”

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Ndipo Absalomu alipomwambia Ahithofeli, “Nishauri; tufanye nini?”

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Absalomu akamwambia Ahithofeli, “Tupe ushauri wako. Tufanye nini?”

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Absalomu akamwambia Ahithofeli, “Tupe shauri lako. Tufanye nini?”

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Kisha Absalomu akamwambia Ahithofeli, Haya, toa ushauri wako, tufanyeje.

Tazama sura
Tafsiri zingine



2 Samueli 16:20
11 Marejeleo ya Msalaba  

Absalomu alipokuwa akitoa dhabihu alituma Ahithofeli Mgiloni, Mshauri wake Daudi, aitwe kutoka mji wake, yaani, Gilo. Njama zao zikawa na nguvu; maana watu waliokuwa pamoja na Absalomu walizidi kuongezeka.


Na tena, Ni nani ambaye yanipasa nimtumikie? Hainipasi kumtumikia mwanawe? Kama nilivyomtumikia baba yako, ndivyo nitakavyokuwa mbele yako.


Naye Ahithofeli akamwambia Absalomu, Ingia wewe kwa masuria wa baba yako, hao aliowaacha ili kutunza nyumba; na Israeli wote watasikia ya kuwa umechukizwa kabisa na baba yako; ndipo itatiwa nguvu mikono yao wote walio pamoja nawe.


Wafalme wa dunia wanajipanga, Na wakuu wanafanya shauri pamoja, Juu ya BWANA, Na juu ya masihi wake,


Haya! Na tuwatendee kwa akili, wasije wakaongezeka; tena, ikitokea vita, wao nao wasije wakashikamana na adui zetu na kupigana nasi, na kutoka katika nchi hii.


Hapana hekima, wala ufahamu, Wala shauri, juu ya BWANA.


Ole wao wanaojitahidi kumficha BWANA mashauri yao, na matendo yao yamo gizani, nao husema, Ni nani atuonaye? Nani atujuaye?


Fanyeni shauri pamoja, nalo litabatilika; Semeni neno, lakini halitasimama; Kwa maana Mungu yu pamoja nasi.


Na ilipokuwa asubuhi, wakuu wa makuhani wote na wazee wa watu wakafanya shauri juu ya Yesu, wapate kumwua;