Ahimidiwe Mungu Aliye Juu Sana, aliyewatia adui zako mikononi mwako. Abramu akampa fungu la kumi la vitu vyote.
2 Mambo ya Nyakati 13:16 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC Wana wa Israeli wakakimbia mbele ya Yuda; naye Mungu akawaua mikononi mwao. Matoleo zaidiBiblia Habari Njema Watu wa Israeli waliwakimbia watu wa Yuda naye Mungu akawatia mikononi mwao. Biblia Habari Njema - BHND Watu wa Israeli waliwakimbia watu wa Yuda naye Mungu akawatia mikononi mwao. Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza Watu wa Israeli waliwakimbia watu wa Yuda naye Mungu akawatia mikononi mwao. Neno: Bibilia Takatifu Waisraeli wakakimbia mbele ya Yuda, naye Mungu akawatia mikononi mwao. Neno: Maandiko Matakatifu Waisraeli wakakimbia mbele ya Yuda, naye Mungu akawatia Israeli mikononi mwao. BIBLIA KISWAHILI Wana wa Israeli wakakimbia mbele ya Yuda; naye Mungu akawaua mikononi mwao. |
Ahimidiwe Mungu Aliye Juu Sana, aliyewatia adui zako mikononi mwako. Abramu akampa fungu la kumi la vitu vyote.
Abiya na watu wake wakawapiga mapigo makuu; hata wakaanguka wameuawa wa Israeli elfu mia tano, watu wateule.
Je! Hao Wakushi na Walubi hawakuwa jeshi kubwa mno, wenye magari na wapanda farasi wengi sana? Lakini, kwa kuwa ulimtegemea BWANA, aliwatia mkononi mwako.
Kutoka Aroeri iliyo katika ukingo wa bonde la Arnoni, na huo mji ulio ndani ya bonde, mpaka kufika Gileadi, hapakuwa na mji uliokuwa na ngome ndefu ya kutushinda; BWANA, Mungu wetu, aliiweka wazi yote mbele yetu; ila nchi ya wana wa Amoni hukuisongelea;
Basi BWANA, Mungu wetu, akamtia mikononi mwako na Ogu mfalme wa Bashani, na watu wake wote; tukampiga, asibakizwe yeyote.
Ndipo Yoshua akanena na BWANA katika siku hiyo ambayo BWANA aliwatoa Waamori mbele ya wana wa Israeli; akasema mbele ya macho ya Israeli, Wewe Jua, simama kimya juu ya Gibeoni; Na wewe Mwezi, simama katika bonde la Aiyaloni.
Kisha BWANA akawapa raha pande zote, sawasawa na hayo yote aliyokuwa amewaapia baba zao; wala katika adui zao wote hakusimama hata mtu mmoja miongoni mwao mbele zao; yeye BWANA akawatia adui zao wote mikononi mwao.
Yuda akakwea; naye BWANA akawatia Wakanaani na Waperizi mkononi mwao; nao wakawapiga huko Bezeki watu elfu kumi.
BWANA, Mungu wa Israeli, akamtia Sihoni na watu wake wote mikononi mwa Israeli, nao wakawapiga; basi Israeli wakaimiliki hiyo nchi ya Waamori, waliokaa katika nchi hiyo.
Kisha Sauli aliambiwa ya kwamba Daudi amefika Keila. Sauli akasema, Mungu amemtia mkononi mwangu; kwa maana amefungwa ndani, kwa vile alivyoingia katika mji wenye malango na makomeo.