1 Wakorintho 5:9 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC Niliwaandikia katika barua yangu, kwamba msichangamane na wazinzi. Matoleo zaidiBiblia Habari Njema Niliwaandikia katika barua yangu msishirikiane na wazinzi. Biblia Habari Njema - BHND Niliwaandikia katika barua yangu msishirikiane na wazinzi. Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza Niliwaandikia katika barua yangu msishirikiane na wazinzi. Neno: Bibilia Takatifu Niliwaandikia katika waraka wangu kuwa msishirikiane na wazinzi. Neno: Maandiko Matakatifu Niliwaandikia katika waraka wangu kuwa msishirikiane na wazinzi. BIBLIA KISWAHILI Niliwaandikia katika barua yangu, kwamba msichangamane na wazinzi. |
Sisemi msichangamane kabisa na wazinzi wa dunia hii, au na wenye kutamani, au na wanyang'anyi, au na wenye kuabudu sanamu; maana hapo ingewalazimu kutoka katika dunia.
Nanyi mwajivuna, wala hamkusikitika, ili kwamba aondolewe miongoni mwenu huyo aliyetenda jambo hilo.
Basi, jisafisheni, mkatoe ile chachu ya kale, mpate kuwa donge jipya, kama vile mlivyo hamkutiwa chachu. Kwa maana Pasaka wetu amekwisha kutolewa kuwa sadaka, yaani, Kristo;
Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa; kwa maana pana urafiki gani kati ya haki na uasi? Tena pana shirika gani kati ya nuru na giza?
Kwa hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha.
Na ikiwa mtu awaye yote halishiki neno letu la barua hii, jihadharini na mtu huyo, wala msizungumze naye, apate kutahayari;
Ndugu, tunawaagiza katika jina la Bwana Yesu Kristo, jitengeni nafsi zenu kutoka kwa kila ndugu aendaye bila utaratibu, wala si kwa kufuata mapokeo mliyoyapokea kwetu.