Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




1 Wakorintho 13:7 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mwenye upendo huvumilia yote, huamini yote, na hustahimili yote.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mwenye upendo huvumilia yote, huamini yote, na hustahimili yote.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mwenye upendo huvumilia yote, huamini yote, na hustahimili yote.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Upendo huvumilia yote, huamini yote, hutumaini yote, hustahimili yote.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Upendo huvumilia yote, huamini yote, hutumaini yote, hustahimili yote.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote.

Tazama sura
Tafsiri zingine



1 Wakorintho 13:7
29 Marejeleo ya Msalaba  

Yakobo akatumika miaka saba kwa kumpata Raheli. Ikawa machoni pake kama siku chache tu kwa vile alivyompenda.


Tazama, ataniua; sina tumaini; Ila hata hivyo nitaithibitisha njia yangu mbele yake.


Unifundishe akili na maarifa, Maana nimeyaamini maagizo yako.


Kuchukiana huleta fitina; Bali kupendana husitiri makosa yote.


Nanyi mtakuwa mkichukiwa na watu wote kwa ajili ya jina langu; lakini mwenye kuvumilia hata mwisho, ndiye atakayeokoka.


Yesu akamwambia, Ukiweza! Yote yawezekana kwake aaminiye.


Basi imetupasa sisi tulio na nguvu kuuchukua udhaifu wao wasio na nguvu, wala haitupasi kujipendeza wenyewe.


Kwa maana tuliokolewa kwa tumaini; lakini kitu kilichotumainiwa kikionekana, hakiwi tumaini tena. Kwa maana ni nani anayekitumainia kile akionacho?


Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni;


Ikiwa wengine wanashiriki uwezo huu juu yenu, sisi si zaidi? Lakini hatukuutumia uwezo huo; bali twayavumilia mambo yote tusije tukaizuia Habari Njema ya Kristo.


Mchukuliane mizigo na hivyo kuitimiza sheria ya Kristo.


Nami wakati ule niliwaambia, nikasema, Mimi siwezi kuwachukua peke yangu.


kwani alimkuta kondeni; yule binti aliyeposwa akalia, pasiwe na mtu wa kumwokoa.


Hata na sisi wenyewe tunaona fahari juu yenu katika makanisa ya Mungu kwa ajili ya subira yenu, na imani mliyo nayo katika adha zenu zote na dhiki mnazostahimili.


Tena haimpasi mtumwa wa Bwana kuwa mgomvi; bali kuwa mwanana kwa watu wote, awezaye kufundisha, mvumilivu;


na upendo, na subira; tena na adha zangu na mateso, mambo yaliyonipata katika Antiokia, katika Ikonio, na katika Listra, kila namna ya adha niliyoistahimili, naye Bwana aliniokoa katika hayo yote.


Bali wewe, uwe mwenye kiasi katika mambo yote, vumilia mabaya, fanya kazi ya mhubiri wa Injili, timiza huduma yako kwa ukamilifu.


Basi na tutoke tumwendee nje ya kambi, tukichukua shutuma yake.


Heri mtu astahimiliye majaribu; kwa sababu akiisha kukubaliwa ataipokea taji la uzima, Bwana aliyowaahidia wampendao.


Yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti, tukiwa wafu kwa mambo ya dhambi, tuwe hai kwa mambo ya haki; na kwa kupigwa kwake mliponywa.


Zaidi ya yote iweni na bidii kubwa katika kupendana; kwa sababu upendano husitiri wingi wa dhambi.