Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




1 Wakorintho 13:6 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli;

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

hafurahii uovu, bali hufurahia ukweli.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

hafurahii uovu, bali hufurahia ukweli.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

hafurahii uovu, bali hufurahia ukweli.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Upendo haufurahii mabaya bali hufurahi pamoja na kweli.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Upendo haufurahii mabaya bali hufurahi pamoja na kweli.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli;

Tazama sura
Tafsiri zingine



1 Wakorintho 13:6
27 Marejeleo ya Msalaba  

Maana mdhalimu hujisifia tamaa ya nafsi yake, Na mwenye choyo humkana BWANA na kumdharau.


Macho yangu yachuruzika mito ya machozi, Kwa sababu hawaitii sheria yako.


Yethro alifurahi kwa ajili ya wema wote BWANA aliowatendea Israeli, kwa alivyowaokoa mikononi mwa Wamisri.


Wapumbavu huidharau hatia; Bali upo upendeleo kwa wenye haki.


Bali kama hamtaki kusikia, roho yangu italia kwa siri, kwa sababu ya kiburi chenu; na jicho langu litalia sana na kutoka machozi mengi, kwa kuwa kundi la BWANA limechukuliwa mateka.


Maana nimesikia shutuma za watu wengi; hofu ziko pande zote. Rafiki zangu wote, wanaonivizia nisite, husema, Mshitaki, nasi tutamshitaki, huenda akahadaika, nasi tutamshinda, tutajilipiza kisasi kwake.


Laiti kichwa changu kingekuwa maji, na macho yangu kuwa chemchemi ya machozi, ili nipate kulia mchana na usiku kwa ajili yao waliouawa wa binti ya watu wangu!


Hujilisha dhambi ya watu wangu, hujifurahisha moyo kwa uovu wao.


Humfurahisha mfalme kwa uovu wao, na wakuu wao kwa uongo wao.


Usifurahi juu yangu, Ee adui yangu; niangukapo, nitasimama tena; nikaapo gizani, BWANA atakuwa nuru kwangu.


Hata akipata kumwona, amin, nawaambia, amfurahia huyo zaidi, kuliko wale tisini na tisa wasiopotea.


Wakafurahi, wakapatana naye kumpa fedha.


ambao wakijua sana hukumu ya haki ya Mungu, ya kwamba wayatendao hayo wamestahili mauti, wanatenda hayo, wala si hivyo tu, bali wanakubaliana nao wayatendao.


Pendo na lisiwe na unafiki lichukieni lililo ovu, mkilishika lililo jema.


Yadhuru nini? Lakini kwa njia zote, ikiwa ni kwa hila, au ikiwa ni kwa kweli, Kristo anahubiriwa; na kwa hiyo nafurahi, naam, nami nitafurahi.


sikuzote kila niwaombeapo ninyi nyote nikisema sala zangu kwa furaha,


Maana wengi huenda, ambao nimewaambieni mara nyingi habari zao, na sasa nawaambia hata kwa machozi, kuwa ni adui za msalaba wa Kristo;


ili wahukumiwe wote ambao hawakuiamini kweli, bali walikuwa wakijifurahisha katika udhalimu.


Nilifurahi mno kwa kuwa nimewaona baadhi ya watoto wako wanaenenda katika kweli, kama vile tulivyopokea amri kwa Baba.