Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




1 Wakorintho 12:6 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Kisha kuna uwezo tofauti wa kutenda kazi, bali Mungu ni yeye yule azitendaye kazi zote katika wote.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Kuna namna mbalimbali za kufanya kazi ya huduma, lakini Mungu ni mmoja, anayewezesha kazi zote katika wote.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Kuna namna mbalimbali za kufanya kazi ya huduma, lakini Mungu ni mmoja, anayewezesha kazi zote katika wote.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Kuna namna mbalimbali za kufanya kazi ya huduma, lakini Mungu ni mmoja, anayewezesha kazi zote katika wote.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Kisha kuna tofauti za kutenda kazi, lakini ni Mungu yule yule atendaye kazi zote kwa watu wote.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Kisha kuna tofauti za kutenda kazi, lakini ni Mwenyezi Mungu yule yule atendaye kazi zote kwa watu wote.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Kisha kuna uwezo tofauti wa kutenda kazi, bali Mungu ni yeye yule azitendaye kazi zote katika wote.

Tazama sura
Tafsiri zingine



1 Wakorintho 12:6
12 Marejeleo ya Msalaba  

Tazama, hayo yote ni Mungu anayeyafanya, Mara mbili, naam, hata mara tatu, kwa mtu,


Akawajibu, Baba yangu anatenda kazi hata sasa, nami ninatenda kazi.


lakini kazi hizi zote huzitenda Roho huyo mmoja, yeye yule, akimgawia kila mtu peke yake kama apendavyo yeye.


Tena kuna huduma tofauti, na Bwana ni yeye yule.


Basi, vitu vyote vikiisha kutiishwa chini yake, ndipo Mwana mwenyewe naye atatiishwa chini yake yeye aliyemtiishia vitu vyote, ili kwamba Mungu awe yote katika wote.


Hivyo, apandaye si kitu, wala atiaye maji, bali Mungu akuzaye.


Mungu mmoja, naye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote na katika yote na ndani ya yote.


Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema.


Nami najitaabisha kwa neno lilo hilo, nikijitahidi kwa kadiri ya kutenda kazi kwake atendaye kazi ndani yangu kwa nguvu.


Hapo hapana Mgiriki wala Myahudi, kutahiriwa wala kutotahiriwa, mgeni wala mshenzi, mtumwa wala muungwana, bali Kristo ni yote, na katika yote.


awafanye ninyi kuwa wakamilifu katika kila tendo jema, mpate kuyafanya mapenzi yake, naye akifanya ndani yetu lipendezalo mbele zake, kwa Yesu Kristo; utukufu una yeye milele na milele. Amina.