Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




1 Wafalme 17:22 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

BWANA akaisikia sauti ya Eliya; na roho ya mtoto ikamrudia, akafufuka.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mwenyezi-Mungu akasikiliza ombi la Elia; mtoto akaanza kupumua tena.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mwenyezi-Mungu akasikiliza ombi la Elia; mtoto akaanza kupumua tena.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mwenyezi-Mungu akasikiliza ombi la Elia; mtoto akaanza kupumua tena.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Mwenyezi Mungu akasikia kilio cha Ilya, na roho ya kijana ikamrudia, naye akafufuka.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

bwana akasikia kilio cha Ilya, na roho ya kijana ikamrudia, naye akafufuka.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

BWANA akaisikia sauti ya Eliya; na roho ya mtoto ikamrudia, akafufuka.

Tazama sura
Tafsiri zingine



1 Wafalme 17:22
12 Marejeleo ya Msalaba  

Eliya akamtwaa mtoto, akamchukua toka ghorofani mpaka chini ya nyumba ile, akampa mama yake. Eliya akanena, Tazama, mwanao yu hai.


Ikawa, walipokuwa wakimzika mtu, angalia, waliona kikosi; wakamtupa yule mtu kaburini mwa Elisha; mara yule maiti alipoigusa mifupa ya Elisha, alifufuka, akasimama kwa miguu.


Akakaribia, akaligusa jeneza; wale waliokuwa wakilichukua wakasimama. Akasema, Kijana, nakuambia, Inuka.


Akamshika mkono, akapaza sauti, akisema Kijana, inuka.


Naye akiisha kusema hayo, akalia kwa sauti kuu, Lazaro, njoo huku nje.


Wakamleta yule kijana, akiwa mzima, wakafarijika faraja kubwa sana.


Maana Kristo alikufa akawa hai tena kwa sababu hii, awamiliki waliokufa na walio hai pia.


Fahamu sasa ya kuwa Mimi, naam, Mimi ndiye, Wala hapana Mungu mwingine ila Mimi; Naua Mimi, nahuisha Mimi, Nimejeruhi, tena naponya; Wala hapana awezaye kuokoa katika mkono wangu,


Wanawake walipokea wafu wao waliofufuliwa. Lakini wengine waliumizwa vibaya hata kuuawa, wasikubali ukombozi, ili wapate ufufuo ulio bora;


Na baada ya siku hizo tatu u nusu, roho ya uhai itokayo kwa Mungu ikawaingia, wakasimama kwa miguu yao; na hofu kuu ikawaangukia watu waliowatazama.


BWANA huua, naye hufanya kuwa hai; Hushusha hadi kuzimu, tena huleta juu.