Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




1 Mambo ya Nyakati 26:13 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Nao wakapigiwa kura kwa ajili ya kila lango, wadogo na wakubwa kwa pamoja, kwa kufuata koo za baba zao.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Kila jamaa, bila kujali wingi, ilipiga kura kuchagua lango watakalosimamia.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Kila jamaa, bila kujali wingi, ilipiga kura kuchagua lango watakalosimamia.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Kila jamaa, bila kujali wingi, ilipiga kura kuchagua lango watakalosimamia.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Kura zilipigwa kwa kila lango, kufuatana na jamaa zao, wakubwa kwa wadogo.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Kura zilipigwa kwa kila lango, kufuatana na jamaa zao, wakubwa kwa wadogo.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Nao wakapigiwa kura kwa ajili ya kila lango, wadogo na wakubwa kwa pamoja, kwa kufuata koo za baba zao.

Tazama sura
Tafsiri zingine



1 Mambo ya Nyakati 26:13
5 Marejeleo ya Msalaba  

Hao nao wakapigiwa kura vile vile, kama ndugu zao wana wa Haruni, machoni pa Daudi mfalme, na Sadoki, na Ahimeleki, na wakuu wa koo za baba za makuhani na za Walawi; koo za baba za mkuu, vile vile kama za nduguye mdogo.


Ndivyo walivyogawanyika kwa kura, wao kwa wao; kwani kulikuwa na wakuu wa patakatifu, na watumishi wa Mungu, wa wana wa Eleazari, na wa wana wa Ithamari pia.


Wakapigiwa kura ya huduma zao, kwa pamoja, mdogo kwa mkubwa, mwalimu kwa mwanafunzi.


Katika hao zilikuwa zamu za mabawabu, yaani, katika hao wakuu, wenye huduma kama ndugu zao, wa kutumika katika nyumba ya BWANA.


Kura ya lango la mashariki ikamwangukia Meshelemia. Ndipo wakamtupia kura Zekaria mwanawe, mshauri mwenye busara; na kura yake ikamtokea ya kaskazini.