Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




1 Mambo ya Nyakati 19:9 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Wakatoka wana wa Amoni, wakajipanga kwa vita langoni pa mji; na hao wafalme waliokuja walikuwa peke yao uwanjani.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Waamoni walitoka wakajipanga kwenye lango la mji, hali wale wafalme waliokuja walikuwa peke yao kwenye tambarare.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Waamoni walitoka wakajipanga kwenye lango la mji, hali wale wafalme waliokuja walikuwa peke yao kwenye tambarare.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Waamoni walitoka wakajipanga kwenye lango la mji, hali wale wafalme waliokuja walikuwa peke yao kwenye tambarare.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Waamoni wakatoka, wakajipanga wakiwa tayari kwa vita langoni la mji wao, wakati wale wafalme wengine waliokuja nao walijipanga kwa vita uwanjani.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Waamoni wakatoka wakajipanga wakiwa tayari kwa vita langoni la mji wao, wakati wale wafalme wengine waliokuja nao walijipanga kwa vita uwanjani.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Wakatoka wana wa Amoni, wakajipanga kwa vita langoni pa mji; na hao wafalme waliokuja walikuwa peke yao uwanjani.

Tazama sura
Tafsiri zingine



1 Mambo ya Nyakati 19:9
12 Marejeleo ya Msalaba  

Waamoni wakatoka, wakapanga vita mahali pa kuingilia lango; na Washami wa Soba, na wa Rehobu, na watu wa Tobu, na wa Maaka, walikuwa peke yao uwandani.


Mfalme akawaambia, Yaliyo mema machoni penu ndiyo nitakayofanya. Basi mfalme akasimama kando ya lango, na hao watu wakatoka kwa maeelfu yao na mamia yao.


Basi, Ben-hadadi mfalme wa Aramu akakusanya jeshi lake lote; nao walikuwapo wafalme thelathini na wawili pamoja naye, na farasi, na magari: akakwea akauhusuru Samaria, akaupiga vita.


Ufanye neno hili; uwaondoe hao wafalme, kila mtu atoke mahali pake, ukaweke majemadari mahali pao.


Basi Yoabu alipoona ya kwamba wamejipanga kwa vita juu yake mbele na nyuma, akachagua baadhi ya wateule wote wa Israeli, akawapanga juu ya Washami.


Basi Daudi aliposikia habari akamtuma Yoabu, na jeshi lote la mashujaa.


Abiya akapanga vita akiwa na jeshi la watu hodari wa vita, watu wateule elfu mia nne; naye Yeroboamu akapanga vita juu yake akiwa na watu wateule elfu mia nane, waliokuwa wanaume mashujaa.


Asa akatoka kukutana naye, wakapanga vita Maresha bondeni mwa Sefatha.


Naye atakuwa roho ya hukumu ya haki kwake yeye aketiye ili ahukumu; naye atakuwa nguvu kwao walindao langoni.


Wanashika upinde na mkuki; Ni wakatili, hawana huruma; Sauti yao inanguruma kama bahari, Nao wamepanda farasi; Kila mmoja amejipanga kama aendaye vitani, Juu yako, Ee binti Babeli.


Kama mshindo wa magari ya vita juu ya vilele vya milima, ndivyo warukavyo; kama mshindo wa miali ya moto iunguzapo mabua makavu, kama mashujaa waliopangwa tayari kwa vita.


Naye Sauli na watu wa Israeli wakakusanyika, wakatua katika bonde la Ela, nao wakapanga vita juu ya hao Wafilisti.